Showing posts with label Jamii. Show all posts
Showing posts with label Jamii. Show all posts

Friday, May 20, 2016

Atiwa Mbaroni Kwa Kumbaka Mtoto wa Miaka 7

Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma linamshikilia mkazi wa eneo la Bombambili, Manispaa ya Songea kwa tuhuma za kukutwa akimbaka mtoto wa miaka saba anayesoma darasa la pili. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Zuber Mwombeji alisema mtuhumiwa alitenda kosa hilo Mei 18 mwaka huu saa 11 jioni...
Share:

Wednesday, May 18, 2016

Waliombaka na Kumlawiti Binti wa Miaka 21 Morogoro Wapandishwa Kizimbani

WATU sita wanaodaiwa kumbaka na kumlawiti msichana kisha kumrekodi na kusambaza video hiyo, leo wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro. Miongoni mwa watuhumiwa hao ni pamoja na Iddi Adamu Mabena (32) Mkazi wa Njombe na Zuberi Thabiti (30) Mkazi wa Mbalali, Mbeya ambapo kesi hiyo...
Share:

Mtoto wa Chacha Wangwe Abadili Msimamo Mahakamani

Mtoto wa aliyekuwa mwanasiasa machachari na Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe, amebadili msimamo mahakamani katika kesi ya kuchapisha taarifa za uongo kupitia mtandao wa kijamii, kuwa Zanzibar inakandamizwa na Tanzania Bara na kwamba ni koloni lake. Mtoto huyo, Bob Chacha Wangwe (24),...
Share:

Tuesday, May 17, 2016

Bodaboda Wagongana Jijini Mwanza, mmoja afariki

Mwendesha pikipiki ambaye hajafahamika amefariki dunia baada kugongana uso kwa uso na mwenzake, eneo la Mabatini jijini Mwanza. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema bodaboda mwingine Stanley Maimu (24), alijeruhiwa katika tukio hilo lililotokea Mei 15. Msangi ...
Share:

Mjane Aliyemwaga Machozi Mbele ya Rais Magufuli Akabidhiwa Nyumba Yake

Hatimaye mjane aliyemwaga machozi mbele ya Rais John Magufuli akidai kudhulumiwa mali ya urithi, amepewa nyumba na shamba baada ya Mkuu wa Wilaya ya Babati mkoani Manyara, Crispin Meela kusuluhisha mgogoro wa umiliki wa mali hizo. Hivi karibuni akiwa mjini Babati, Rais Magufuli alimuagiza...
Share:

Monday, May 16, 2016

Vijana Wanaovaa Suruali Chini ya Kiuno Kuchapwa Viboko 70

Wakazi wa Kata ya Karansi, Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro wametoa uamuzi kuwa wanawake watakaovaa sketi fupi na vijana watakaovalia suruali chini ya kiuno, wataadhibiwa kwa kuchapwa viboko 60 hadi 70. Uamuzi huo umefikiwa na wakazi zaidi ya 200 wakisema uvaaji huo ni kinyume na mila...
Share:

Wanaofanya Biashara ya Ngono Wataka ajira Irasimishwe

Baadhi ya wanawake wanaojiuza katika mitaa ya Majengo B na Fisi, mjini Mpanda mkoani Katavi wameitaka Serikali kuandaa utaratibu wa kuwatambua ili nao waweze kulipa kodi na kuliingizia taifa pato kutokana na shughuli wanayofanya ya kuuza miili yao. Wakizungumza kwa nyakati tofauti juzi...
Share:

Saturday, May 14, 2016

Ahukumiwa Kifungo cha Miaka 30 Jela Kwa Kumuoa Binti Yake wa Kumzaa

Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma, jana ilimhukumu kifungo cha miaka 30, Godfrey Mjelwa (48), baada ya kupatikana na hatia ya kuishi kinyumba na binti yake wa kumzaa. Hakimu Mkazi katika mahakama hiyo, Mwajuma Lukindo alisema ushahidi wa pande zote ulithibitisha kuwa mtuhumiwa alitenda...
Share:

Friday, May 13, 2016

Mbuzi wa Tambiko Aua Watu Watano wa Familia Moja

VILIO, simanzi na hofu vimetanda kwa wakazi wa Kitongoji cha Lotii, Kijiji cha Mwitikira, Tarafa ya Olboloti, Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara baada ya watu watano wa familia moja kufariki dunia kwa namna ya kutatanisha.   Watu hao wanadaiwa kufikwa na mauti baada ya kula nyama ya mbuzi iliyotolewa...
Share:

Thursday, May 12, 2016

Mtoto wa marehemu, Chacha Wangwe afikishwa kortini kwa makosa ya kimtandao

BOB Chacha Wangwe (24), mtoto wa mwanasiasa marehemu Chacha Wangwe, amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa tuhuma za kuchapisha taarifa za uongo katika mitandao ya kijamii. Akisoma kesi hiyo namba 167, Paul Kagoshi mbele ya Waliarandwe Rema, Hakimu Mkazi katika mahakama...
Share:

Monday, May 9, 2016

Atupwa Jela Miaka 33 kwa Wizi

Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Chato mkoani Geita, imemhukumu kifungo cha miaka 33 jela Matiku Wambura (34) baada ya kupatikana na hatia ya makosa manne ya wizi likiwamo la kuiba vyombo vya muziki mali ya Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA) Chato mission. Wambura ambaye ni mkazi wa Kijiji...
Share:

Monday, May 2, 2016

Video: Godfrey Magila Aeleza Jinsi Ilivyo Rahisi Kukamatwa kwa Mtu Yeyote Anayefanya Makosa ya Kimtandao

Godfrey Magila ni mtaalamu wa Teknolojia kwenye upande wa mitandao na ndio aliyetengeneza App ya Tigo Back-Up, amekaa kwenye Interview na Millard Ayo na kueleza urahisi wa kukamatwa kwa yeyote anaefanya kosa la kimtandao ikiwa tayari sheria ya makosa ya kimtandao imeshaanza kufanya kazi...
Share:

Wednesday, April 27, 2016

Hali ya Kituo cha Mabasi ya Kusini Mbagala si Shwari

 Hali ya kituo kikuu cha Mabasi yaendayo mikoa ya Kusini ya Lindi na Mtwara si nzuri jambo ambalo limekuwa kero kwa abiria pamoja na watoa huduma hiyo ya usafiri. Kituo hicho kilichopo Mbagala Rangi Tatu jijini Dar es Salaam kimesheheni madibwi ya maji hivyo wadau mbalimbali wameiomba...
Share:

Thursday, October 1, 2015

Magufuli Afunika Dodoma.....Aahidi Kumaliza Mapigano Ya Wakulima Na Wafugaji

Mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dkt. John Pombe Magufuli (pichani) akihutubia umati wa watu kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma jana. Akitoa hotuba yake katika mji wa Kibaigwa Dk. John Pombe Magufuli alisema hakuna kitu...
Share:

Wednesday, September 30, 2015

Polisi Wasambaratisha utafiti wa Nani Mkali kati ya LOWASSA na MAGUFULI Uliokuwa Ukifanywa Mitaani

Wakati tafiti za kienyeji zenye lengo la kupima kukubalika kwa wagombea urais, hasa Dk John Magufuli na Edward Lowassa zikizidi kuongezeka, polisi jijini Arusha mwishoni mwa wiki walitumia nguvu kutawanya vijana waliokuwa wakiendesha kura za maoni kwenye stendi ndogo ya mabasi na soko kuu. Tangu ...
Share:

Thursday, May 28, 2015

Update: Yule msichana aliyeua mtoto wa miaka 9 afikishwa mahakamani....Apigwa ngumi mbele ya polisi huko morogoro

Msichana Judith Chomile(15) amefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Morogoro akikabiliwa na tuhuma za kumnyonga hadi kufa mtoto mwenye umri wa miaka 9 mwanafunzi wa darasa la tatu katika shule ya msingi Bernard Benderi ya mjini Morogoro. Akisoma shitaka mbele ya hakimu mkazi Ivan Msaki,...
Share:

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © 2025 GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger