Showing posts with label wasanii. Show all posts
Showing posts with label wasanii. Show all posts

Friday, May 20, 2016

Video: Giggy Money 'Bora Ningetembea Na Marehemu Kinyambe Kuliko Nay wa Mitego'




 Credit: GlobalPublishers
Share:

Diamond Atajwa Kuwania Tuzo za BET 2016



Diamond Platinumz anaendelea kupaa katika ulimwengu wa muziki kimataifa ambapo mwaka huu pia nyota yake imeng’aa kwenye tuzo kubwa za Black Entertainment Television (BET 2016).

Mwimbaji huyo ametajwa kuwania kipengele cha Best International Act: Africa akichuana na wasanii wengine nguli Afrika ambao ni pamoja na AKA kutoka Afrika Kusini, Cassper Nyovest wa Afrika Kusini Black Cofee wa Afrika Kusini, Yemi Alade wa Nigeria, Wizkid wa Nigeria, Mzvee wa Ghana na Serge Beynaud wa Ivory Coast.

Share:

Gardner Amjibu Lady JayDee Kuhusu Kumtaka Kumuomba Radhi Hadharani

Hatimaye mtangazaji wa Clouds Fm, Gardner G. Habash amemjibu aliyekuwa mkewe, Lady Jay Dee, aliyemtaka aombe radhi ndani ya siku saba kwa kauli aliyoitoa iliyodaiwa kuwa imelenga kumdhalilisha. Katika majibu yake amekana madai hayo.

Siku chache zilizopita, Gardner alionekana katika kipande cha Video akisherehesha tukio la kumsaka mrimbwende wa chuo cha Tanzania Institute of Accountancy (TIA) jijini Dar es Salaam, ambapo alisema kuwa “yule binti sina tatizo naye, nimeshamkojoza kwa miaka kama 15 hivi…”, kisha wimbo wa ‘Ndindindi’ wa Jay Dee ukachezwa na DJ.

Kama ilivyokuwa kwa Lady Jay Dee aliyetoa siku saba za kuombwa radhi kupitia kwa mwanasheria wake Amani Tenga, Gardner amejibu kupitia mwanasheria wake Stephen Axwesso.
 
Katika barua yake kwa mwanasheria wa Lady Jay Dee, mwanasheria huyo wa Gardner amekiri kuwa ni kweli mteja wake alizungumza maneno hayo alipokuwa katika shughuli iliyotajwa, lakini alidai kuwa hakuna sehemu aliyomtaja mkewe huyo wa zamani.

Alisema kuwa madai ya upande wa Lady Jay Dee hayana mashiko na alimshauri mwanasheria huyo kupitia upya sheria inayozungumzia wanandoa waliotalakiana ili aweze kumshauri vizuri mteja wake kuhusu suala hilo.

Nakala ya barua hiyo pia imetumwa Clouds Media Group na kwa Rais wa Wanafunzi wa Chuo cha TIA.



Share:

Thursday, May 19, 2016

Wema Sepetu Afunguka Haya Kuhusu Alikiba

Msanii wa filamu nchini Wema Sepetu amefunguka na kusema kuwa msanii Alikiba ni mtu wa kumuacha kutokana na uwezo wake wa kuimba na namna ambavyo anaweza kuipangilia sauti yake kwenye muziki.

Wema Sepetu amezidi kuonyesha mapenzi aliyonayo kwenye kazi za msanii Alikiba na kusema huwa zinamkosha sana na kudai hajawahi kumuangusha siku zote.

“Ila huyu bichwa wangu mimi ananikoshaga sana. Na mumuachage tu kwakweli. Bichwa una sifa lakini maana si kwa Vocal hizi. Halafu mimi siwezi kukubania namba bana. Naupenda sana huu wimbo jamani. Wajua kutukunaga mashabiki wako. Good work Bichwa wangu Officialalikiba did it again ladiez & Gentlemen” aliandika Wema Sepetu

Mbali na hilo Wema Sepetu amempa pongezi msanii Alikiba kwa kuweza kusaini mkataba chini ya kampuni ya muziki ya ‘Sony Music’ na kusema kuwa alistahili hilo na zaidi ya hilo kwani anakipaji kikubwa.

”God Grants accordingly… Congrats Bichwa wangu for that Big Contract… You deserve it & more… Time Heals all wounds… The Sky remains to be the only Limit for u baba…”
Share:

Ali Kiba Asaini Mkataba na Kampuni kubwa ya Muziki duniani ya Sony jijini Johannesburg, Afrika Kusini

Mwimbaji staa wa bongofleva Alikiba leo amesaini mkataba na  Sony Music , kampuni kubwa ya muziki inayofanya kazi na mastaa wa dunia kama Beyonce, John Legend na Chris Brown.

Moja ya kazi za mkataba huo ni kumtengeneza Alikiba kweye kiwango cha juu zaidi kimuziki, kibiashara na kugharamia video zake na anaporekodi audio zake, kila anapotoa muziki mpya unaachiwa kwa nguvu ya usimamizi wa Sony Music kwenye masoko makubwa ya muziki kama Marekani, Ulaya na Africa.

Mkataba  huo aliosaini Ali kiba unafanana  na ule aliosaini mwimbaji staa wa Nigeria Davido ambapo unavipengele vya kusababisha kolabo kwa urahisi zaidi na mastaa wakubwa wakiwemo wa Marekani.



Share:

Rose Ndauka Atoa Siri ya Mambo Yake Kumnyookea

 MKALI wa filamu Bongo, Rose Ndauka ametoa siri ya mambo yake kumnyookea kuwa imetokana na kumuhusisha Mungu kwa kila anachokifanya na wala si vinginevyo kama watu wanavyodhania.

Akizungumza na Amani, Rose ambaye kwa sasa anamiliki kampuni inayojishughulisha na kutengeneza Jarida la Rozzie, alisema kuwa Mungu ndiye aliyemtendea miujiza hiyo kwani asingemshirikisha asingekuwa hapo alipo.

“Siri kubwa ya mafanikio niliyonayo ni kumtegemea Mungu na hakuna namna yoyote kinyume na hapo niliyofanya. Kuna faida kubwa sana katika maisha yangu, nimeona na nimeshuhudia kabisa, wala sitathubutu kumuacha kamwe,” alisema Rose.
Share:

Nay: Gigy Anatafuta Kiki Kwangu


MKALI wa Ngoma ya Saka Hela, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ ameamua kumfungukia muuza nyago kwenye video za Kibongo, Gift Stanford ‘Gigy Money’ kuwa anatafuta kiki kutumia jina lake katika mahojiano anayofanya na vyombo mbalimbali vya habari.

Akichonga na Showbiz Xtra, Nay alisema kuwa amekuwa akisikia juu ya Gigy akimsema si chochote kwake na kwamba ni mbahili alishawahi kumlipa elfu ishirini baada ya kumaliza kutengeneza video zake.

 “Yaani huyo Gigy anatafuta kiki, namshangaa sana kila sehemu kunisema hovyo, kwanza hatuendani kwa chochote,” alisema Nay.

Hivi karibuni katika mahojiano na Global TV Online, Gigy alisikika akimponda Nay kuwa ni mtu bahili na haitakuja kutokea yupo naye iwe kikazi ama vyovyote kwa kuwa hana hadhi ya kuwa naye.

Share:

Video: Giggy Money Adai kuwa Hata Akiwa Hawara Kwa Matonya Hamna Shida

Story ambazo zilisambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Matonya kwa sasa anatoka kimapenzi na Giggy Money huku wakisikika kuwa ni kick ya ngoma yao ya Supu.

Katika mahojiano waliyofanya na ENewz wote wawili walishindwa kukubali moja kwa moja kuwa wameanguka pamoja kitandani au hawajaanguka kitandani lakini walibaki kusifia Supu huku Giggy Money akisema kuwa Matonya kwake ni zaidi ya mpenzi.
Share:

Shilole: Wanaume Suruali Wasio na Pesa Sasa Basi

MSANII wa Muziki wa Kizazi Kipya, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ amefunguka kuwa kuanzia sasa hataki tena kuwa na mwanaume suruali, bali anahitaji mtu mwenye nazo, ndiyo maana ameamua kufanya kazi kwa bidii.

Akilonga na Risasi Vibes, Shilole alisema kuwa kwa sasa ameamua kukaa singo kwa sababu ameona hakuna faida ya kuwa na mwanaume asiye na kitu.


Kuhusu Nedy Music anayedaiwa kuwa naye mara tu baada ya kumwagana na Nuh Mziwanda, Shishi Baby alisema hana uhusiano naye wa kimapenzi, isipokuwa ni rafiki wa kawaida tu!
Share:

Feza na Lulu Wajitosa Kwenye Bifu ya Vanessa na Shilole

Msanii wa filamu Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Feza Kessy wamejitosa kwenye bifu la Shilole na Vanessa Mdee ambalo linaendelea katika mitandao ya kijamii.
Chanzo cha bifu ya Shilole na Vanessa hakijatambulika, lakini wawili hao toka jana wamekuwa wakirushiana maneno makali na vitisho katika mitandao ya kijamii hali ambayo imewafanya baadhi ya wasanii kuingilia kati sakata hilo la aina yake.

Muigizaji mahiri Elizabeth Michael ‘Lulu’ alikuwa moja kati ya msanii wa kwanza kutupia neno kwenye ugomvi huo kwa namna ya kushangazwa na jinsi watu wanavyosifia uzuri wao kupitia mitandao ya kijamii.

“Hebu nikazane kusoma nianze ligi za kikubwa na dada zangu wenye madegree na ma masters kama ‘Esilovey’ hizi ligi nyingine zinasikitisha,” aliandika Lulu kupitia Twetter huku akiongeza post nyingine kwa kuandika “Watu wanashindania uzuri, makalio, followers, nguo, outings, umaarufu, umaarufu wenyewe kama network ya mtandao unaokuwaga mpya, full kukatakata,”

Pia msanii wa muziki na mtangazaji wa Choice Fm, Feza Kezzy baada ya kuona stori inakuwa kubwa katika mitandao ya kijamii, aliandika ya moyoni kuhusu jinsi watu wanavyo shabikia mambo yasiyo na maana na kuacha kushabikia mambo ya msingi.

“Yaani watu wa ajabu sana, inabidi mbadilike. Watu wakifanya mazuri or kazi nzuri hamsemi, hamsupport, lakini umbea comments karibu laki moja dah. It’s very sad, bongo we need to change and support our talents Not tear them apart, Ntawacheka sana mkigundua labda hata ma star hawa hawana beef lol,” aliandika Feza kupitia instagram.
Share:

Wednesday, May 18, 2016

Vanessa Mdee Vs Shilole Hali ni Tete Instagram, Wapigana Vijembe Laivu


Ni juzi tu tuliona video ya msanii wa kimataifa vanessa mdee akimfundisha yai local artist Shishi baby salon cha ajabu ni leo ghafla wamenza kutupiana maneno uko instagram
shilole alianza na ujumbe huu.


Haikuchukua mda nae vanessa mdee v. money amendika maneno haya kupitia instagram account yake


"Nikupe KICKIII ujulikane au sio? Kila siku twanyamaza ndiyo mtugaragaze. Sit the f**k down. Mimi sio wale uliowazoea. P.s: You ain't worth this post inashushwa sasa hivi" #MessageSent
Share:

Idris Sultan Amwandikia Wema Sepetu Ujumbe Mzito

Uhusiano wao umepitia misukosuko mingi ikiwemo kuachana mara kadhaa lakini Idris Sultan na Wema Sepetu hawajalikatia tamaa pendo lao.

Ni muda mrefu tangu Idris aandike kitu kwenye mitandao ya kijamii kuhusu penzi lake na Wema baada ya kudai wameamua kuuweka uhusiano wao private kwa sasa. Lakini sasa mshindi huyo wa Big Brother Africa ameshare ujumbe mahsusi kwa mpenzi wake huyo.

“I am proud to say the mistakes we have made have not only made us stronger but better, faster, wiser, love too strong, stronger than any of us,” Idris ameandika kwenye picha ya Wema aliyoiweka Instagram.

“We ni kasumbufuuu, unasusasusa, wivu ndo usiseme, kugombana hadi kulia but in the end of the day i will open my arms na utajileta mwenyewe utaniangalia usoni and tell me “I hate you” and lay on my chest. I will smile and say “I love you too”. We have gone through heaven and hell and now you’re my bestfriend, family, wifey, lover you’re my cherry . #WolfQueen.”

Hivi karibuni wawili hao waliingia kwenye matatizo makubwa baada ya video inayomuonesha Wema akimbusu mwanaume mwingine kusambaa mtandaoni. Idris alikiri kuumizwa na jambo hilo.
Share:

Tuesday, May 17, 2016

Faiza Atoa Sababu za Kwanini Hajatoka na Mtanzania Tangu Aachane SUGU


Msanii wa filamu na Mama wa mtoto mmoja aitwae Sasha, Faiza Ally amedai hajawahi kufanya mapenzi na mtanzania yeyote toka aachane na aliyekuwa mume wake Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ kwa madai kuwa anaogopa kuzalilishwa.

Muigizaji huyo amesema hali hiyo imekuja kutokana na matukio ya uzalilishaji wa wanawake ambayo yanaripotiwa kutokea katika sehemu mbalimbali hapa nchini.
Kupitia instagram, Faiza ameandika:

Wanaume acheni kuzalilisha wanawake, video imenisikitisha na mwanamke yoyote atakaye ipost ni mjinga, maana ana chofanya naye ni uzalilishaji. Kusema kweli toka niachane na Baba Sasha sija date na mtanzania Kwa sababu naogopa unaweza ukahisi unatongozwa kwa heri Kumbe mtu kakupania kukuzalilisha! Nimesikitishwa lkn kwa hatua zilizo chukukuliwa na serekali na juhudi za muandishi nimeshukuru sana sana! Na Niko tayari hata kuandamana kupinga wanaume wazalilishaji# na nukuu maneno kutoka bungeni #wanawake ni mama zenu#dada zenu#mabinti zenu#shangazi zenu #ACHENI KUTUZALILISHA
Share:

Monday, May 16, 2016

Gigy Money: Niko Kwenye Uhusiano wa Kimapenzi na Gardner Kwa Miezi 6 Sasa

Muuza sura kwenye video za Kibongo, Gift Stanford ‘Giggy Money’ amefunguka kuwa mtangazaji maarufu Bongo wa Clouds FM, Gardner G. Habash hachomoki kwake na hadi sasa wako kwenye uhusiano wa mapenzi kwa muda wa miezi sita.

Gigy mefunguka haya baada ya picha zinazomuonesha akiwa kwenye mapozi ya kimahaba na Gardner kusambaa kwenye mitandao ya kijamii. Giggy alisema mtangazaji huyo amekuwa mtu wa muhimu kwake kwa sasa.

“Kwani kuna tatizo nikiwa na Gardner? Yule ni mtu muelewa na sahihi kwangu, ninafikiri kupitia yeye nitajifunza mambo mengi na kuzidi kufanikiwa kwa sababu yeye ni moja kati ya watu ambao wako kwenye tasnia ya burudani kwa muda mrefu,” alisema Giggy Money.

Gardner alipotafutwa ili aweze kueleza kuhusu ishu hii alisema:

“Nipo karibu na Giggy lakini hatuna uhusiano wa kimapenzi, kwa hiyo kama anasema hivyo si kweli lakini yeye ni shabiki wangu na mimi ni mshabiki wake, ninapenda pia kazi anazozifanya,”

Share:

Saturday, May 14, 2016

Lady Jay Dee Sasa Kuitafuta Haki yake Kwa Njia ya Mahakama..Amtaka Gadner Kuomba Msamaha Mbele ya Umma


Lady Jay Dee Sasa Kuitafuta Haki yake Kwa Njia ya Mahakama.Amtaka Gadner Kuomba Msamaha Mbele ya Umma la sivyo hatua za kumpeleka Mahakani zitaendelea, Soma Hii Hapa Chini:

Share:

Aunt Ezekiel, Mose Iyobo Pamoja na Mtoto Wao ‘Cookie’ Kuandaa Filamu ya Pamoja


Msanii wa filamu, Aunt Ezekiel na mpenzi wake Mose Iyobo pamoja na mtoto wao ‘Cookie’, wapo kwenye mchakato wa kuandaa filamu ya fimilia.

Mose Iyobo ambaye pia ni dancer wa Diamond, ameiambia Bongo5 kuwa tayari wapo kwenye mchakato wa kauandaa kazi hiyo.

“Kuna kazi za filamu zinakuja, mtaziona tu, tena familia yetu yote mtaiyona,” alisema Mose. “Unajua Cookie yupo kwenye mikono ya Mama muigizaji na Baba dancer, kwa hiyo ingawa mwenyewe anaweza kuchagua kwa kwenda lakini sisi ndiyo taa yake, kwa hiyo mambo yakikaa sawa mtamuona, Cookie, Baba yake na Mama yake kwenye filamu moja,” alisema Mose.

Pia Mose alisema mtoto wao ‘Cookie’ ataonyeshwa kwa mara ya kwanza hadharani tarehe 21 mwezi huu baada ya kutimiza mwaka mmoja.
Share:

Friday, May 13, 2016

TIGO Yakata Rufaa Kupinga Kuwalipa AY na Mwana FA Shilingi Bilioni 2.18

Kampuni ya simu ya MIC Tanzania (Tigo) imekata rufaa kupinga hukumu iliyoamuru iwalipe Sh2 bilioni wanamuziki wawili, Ambwene Yesaya na Hamisi Mwinjuma kutokana na kutumia bila ya ridhaa yao, nyimbo za wasanii hao nyota nchini.

Yesaya, ambaye ni maarufu kwa jina la kisanii la AY na Mwinjuma anayejulikana kwa jina la MwanaFA, walifungua kesi hiyo ya madai kwenye Mahakama ya Wilaya ya Ilala kupinga kitendo cha kampuni hiyo ya huduma za simu kutumia nyimbo zao kwenye miito ya simu bila ya ridhaa yao.

Nyimbo mbili zilizotumika kwenye miito hiyo ya simu ni “Dakika Moja” na “Usije Mjini” ambazo nyota hao wameshirikiana.

Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Juma Hassan alitoa hukumu ya kesi hiyo Aprili 11, akiwapa ushindi wasanii hao maarufu katika muziki wa vijana uliopachikwa jina la Bongo Fleva.

Katika hukumu hiyo, Mahakama iliiamuru Tigo kulipa Sh5 milioni kama faini ya uharibifu na kulipa Sh2.16 bilioni kama faini ya jumla.

Iwapo wasanii hao watashinda rufani hiyo, watakuwa wameandika historia katika matumizi ya Sheria ya Haki Miliki na watakuwa wasanii wa kwanza wa muziki wa kizazi kipya kufungua kesi na kushinda.

Katika rufaa hiyo, Tigo kupitia kampuni ya Law Associates imeainisha sababu saba za rufani, ikidai hakimu wa Mahakama ya Ilala alikosea kisheria kuwapa ushindi wasanii hao kwa kuwa hawakuthibitisha madai yao wala hasara waliyopata.

Kampuni hiyo pia inadai kuwa mbali na kutoeleza hasara waliyoipata kutokana na kazi zao kutumika kwenye miito ya simu, walitakiwa kueleza faida ambayo wangepata kama kazi zao zisingetumika kwenye miito hiyo.

Sababu nyingine ya Tigo kukata rufaa hiyo ni wasanii hao hawakuwa wamesajili kazi zao Chama cha Hakimiliki Tanzania (Cosota).

Tigo inadai kuwa wakati wa usikilizwaji wa kesi ya msingi, wadai walisema wamesajili kazi hizo, lakini waliwasilisha barua ya Baraza la Sanaa (Basata) ya kutambua kupokea kazi zao na si cheti cha usajili cha Cosota.

Kwa mujibu wa Tigo, wanamuziki hao walipaswa kuwasilisha mahakamani cheti cha usajili wa Cosota ambako kuna utaratibu wa kujisajili ikiwa ni pamoja na kujaza fomu maalumu baada ya kulipia malipo ya usajili ya kila mwaka.

Kampuni hiyo inasisitiza kuwa wasanii hao hawakuwa na haki ya kudai fidia hiyo wakati hawajasajili kazi hizo Cosota na hivyo kuiomba Mahakama Kuu itengue hukumu iliyowapa ushindi.

Akizungumzia hukumu iliyowapa ushindi, MwanaFA alisema huu ni wakati wa mabadiliko.

“Wale waliokuwa wanachukulia Sheria ya Hakimiliki kama mzaha, watambue kwamba zama zimebadilika,” alisema nyota huyo wa muziki wa rap ambaye aliingia kwenye muziki akijitambulisha kama Mwanafalsafa kabla ya kufupisha jina lake na kuwa MwanaFA.

“Hakuna anayetilia maanani kutumia kazi za wasanii bila ridhaa yao huku akinufaika na wasanii kubaki wanalialia. Huu ni wakati wa kutambua kuwa inawezekana kupata haki yako iwapo utasimama kidete kuitetea kwa sababu sheria zipo.”

Akisisitiza, AY ambaye pia ni nyota katika muziki wa rap aliyeimba R&B akishirikiana na Diamond katika siku za karibuni, alisema huo ni mwanzo wa wasanii kufunguka masikio na kutambua haki zao.

Alisema wasanii wamekuwa wakilalamika juu ya haki za kazi zao, lakini hawachukui hatua.

“Wakati ni sasa, muziki ni kazi kama kazi nyingine na ni ajira pia, hivyo unastahili kuheshimiwa,” alisema AY
Share:

Ya Snura Yamkuta Gigy Money!


ZIKIWA ni siku chache zimepita tangu staa wa Muziki wa Bongo Fleva, Snura Mushi kufungiwa video yake ya Chura na kutakiwa kuitengeneza upya, Video Queen, Gift Stanford ‘Gigy Money’ naye amejikuta akikumbana na rungu la Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) kufuatia kusambaza kava la video ya wimbo wake mpya lenye picha yake inayomuonesha akiwa mtupu.

Kava hilo la wimbo wake wa Supu ambao alitarajia kuuachia jana, alilisambaza kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii ambapo mashabiki walioiona kwa mara ya kwanza walishangazwa na kitendo hicho kwani picha yake haikumstiri mwili kama yalivyo maadili ya Kitanzania.

“Yaani hawa wasanii ni sikio la kufa, Gigy ameweka kava hili ambalo lina picha yake ya nusu utupu kabisa na limesambaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, hajajifunza kwa mwenzake Snura?” alihoji mdau mtandaoni.

Walipotafutwa Basata na kuulizwa juu ya video queen huyo, Katibu Mtendaji wa Basata, Godfrey Mngereza alisema wao wanasimamia maadili ya Kitanzania hivyo kama Gigy amekiuka, wanampa onyo asiuachie wimbo huo hadi atakapoufanyia marekebisho.

“Kwanza huyo Gigy Money hatumtambui kabisa hapa baraza maana hajajisajili kama msanii na sheria ya mwaka 1984 inasema mtu yeyote hatakiwi kufanya kazi ya sanaa bila kujisajili hivyo hata hao ma-video queen wanatakiwa wajisajili maana hatuwatambui.

“Mtu akikiuka maadili, hatumvumilii na asitegemee kazi yake kupigwa katika vyombo vya habari wala mitandao, tunawasihi wasanii kutoa kazi zenye maadili ili kuepuka usumbufu,” alisema Mngereza.

Alipotafutwa Gigy kuhusiana na suala hilo, alisema:
“Mimi najua ma-video queen hatuhusiani na mambo ya Basata na niseme tu wimbo wangu wuko ndani umetulia, kava lisiwatishe ila nitaenda Basata kufuata utaratibu,” alisema Gigy.
Share:

Picha: Mafikizolo Toka South Na Diamond Platinumz Wafunika Vibaya Tamasha La Vodacom Chuo Kikuu cha Dodoma

Mwanamuziki wa kizazi kipya Nasibu Abdul “Diamond Platinums” pamoja na kundi la muziki la Mafikizolo wakiimba wimbo wao wa Color of Afrika wakati wa Tamasha la Vodacom Kichuo zaidi lillilofanyika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
 
Mwanamuziki wa kizazi kipya Nasibu Abdul “Diamond Platinums” akiwaimbia kwa hisia wakati wa mashabiki wake waliofika kwenye Tamasha la Vodacom Kichuo zaidi lillilofanyika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) jana.
 
Nyomi ya  mashabiki wa muziki waliofika kwenye Tamasha la Vodacom Kichuo zaidi lillilofanyika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
 
Msanii wa muziki wa kundi la Mafikizolo kutoka Afrika ya kusini,Theo  Kgosinkwe  akionyesha umahiri wake wa kucheza muziki  katika Tamala la Vodacom kichuo zaidi lililofanyika  chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) jana
 
Share:

Thursday, May 12, 2016

Update: Kifo cha Msanii wa Uchekeshaji 'KINYAMBE' Kimesababishwa na Uvimbe Tumboni

Mchekeshaji maarufu nchini Tanzania kutoka katika Kundi la Vituko Show, Mohammed Abdallah ‘Kinyambe’ amefariki dunia Jumatano hii baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na uvimbe tumboni.

Taarifa za kifo chake zilianza kuzagaa jana katika mitandao ya kijamii baada ya wasanii wa filamu kuanza kupost picha mbalimbali huku wakiandika RIP Kinyambe.

Akizungumza na Bongo5 Alhamisi hii mmoja kati ya wasanii wanaounda Chama Cha Wasanii Wachekeshaji Tanzania, Mkono Mkonole, amesema Kinyambe amefariki jana akiwa mkoani Mbeya.

“Kinyambe alikuwa anasumbuliwa na uvimbe tumboni kwa muda mrefu, ila jana ndo amefariki akiwa mkoani Mbeya, katika hospitali ya mkoa wa Mbeya,” alisema Mkonole.
Kuhusu taratibu za mazishi, Mkonole amesema bado hawajapanga kwani taarifa za kifo chake wamezipokea jana usiku.

“Kusema kweli bado hatujapanga kuhusu mazishi, lakini sasa hivi tunawasiliana na ndugu zake ili kujua taratibu za mazishi na zikamilika tutaweka wazi,” alisema Mkono.

Kinyambe atakumbukwa kwa uwezo wake wa kuigiza, hasa hasa jinsi anavyoongea pamoja na mtindo wake wa pekee wa kugeuza macho.

Baada ya taarifa hizo, wasanii mbalimbali wa filamu na muziki walishare ya moyoni jinsi walivyozipokea taarifa hizo za kusikitisha.

Riyama Ally

Innalilah wainna ilaihi rajiun mbele yake nyuma yetu kazi yake mola haina makosa mola akueke panapo stahili ndugu yetu Amin #kinyambe wasanii wenzangu rafiki zangu dunia na #dini dunia mapito #DUNIAMALIYAMUNGU BINADAMU #PUMZITU (TUPENDANDE TUHESHIMIANE) MUNGU NDIO KILA KITU . 😢😢😢😢😢😢😢😢😢😢😢😢😢
Raymond
Daaah!!!!! SIAMINI NINACHOKIONA.ULIKUA MTU POA SANA NAKUMBUKA ULIVYOKUA UKINISAPOTI MDOGO WAKO KITAMBO SANA.KAZI YA MOLA HAINA MAKOSA. R.I.P BROTHER MUDI #KINYAMBE
Share:

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger