Monday, May 2, 2016

Magufuli Kufyeka Mishahara ya Maafisa Wakuu, Hakuna Atakayezidi Mshahara wa Milioni 15

Rais wa Tanzania John Magufuli ametangaza kuwa hakuna afisa wa taasisi na mashirika ya umma atakayelipwa mshahara wa zaidi ya shilingi za Tanzania 15 milioni, ambazo ni sawa na dola 6,900 za Marekani.

Akiongea katika uwanja wa Mazaina, mjini Chato, kiongozi huyo alisema agizo hilo litatekelezwa katika mwaka ujao wa kifedha.

Kwa mujibu wa gazeti la The Citizen, Dkt Magufuli alisema si haki kwa Tanzania kuwa na watu katika mashirika ya umma wanaolipwa mishahara ya zaidi ya shilingi za Tanzania 40 milioni wakati wafanyakazi wa ngazi za chini wanalipwa Sh300,000 kila mwezi.

Ilikuwa mara ya kwanza kwa Dkt Magufuli kufanya ziara rasmi mji huo wa nyumbani tangu kuchaguliwa kuwa rais Oktoba mwaka jana.

Alisema mishahara hiyo minono itafyekwa na watu wanaolipwa mishahara ya chini kuongezewa.

Share:
Weka Maoni yako Hapa

Habari Zinginezo:

0 comments:

Post a Comment

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © 2025 GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger