Monday, May 2, 2016

Bilioni 15 Zatengwa Kuwaongezea Ujuzi Vijana

SERIKALI kupitia Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Walemavu) imetenga zaidi ya Sh. 15 Bilioni katika bajeti yake ya 2016/17 kwa ajili ya kuwaongezea vijana ujuzi unaohitajika kwenye soko la ajira.

Jenista Muhagama, waziri wa wizara hiyo amesema hayo leo wakati wa mahojiano maalum na MwanaHalisi Online.

Amesema, kutokana na tatizo la ajira nchini, wameamua kutenga fedha hizo ili kuwawezesha vijana kupata mafunzo katika maeneo mbalimbali ili waweze kuzalisha.

Amesema, wamegundua nguvu kazi ambayo iliyopo haiendani na soko la ajira na kwamba, miongoni mwa sekta zinazoongoza katika kuinua uchumi ni kilimo, miundombinu, viwanda, hoteli, mafuta na gesi.

“Kwa hiyo sisi lazima tuwatayarishe vijana wetu wa Tanzania, ni ngazi ngapi za ajira zitatakiwa? wakihitajika mafundi wa kuchomea mabomba ni lazima  vijana wetu wakapate ajira,” amesema Muhagama na kuongeza;

“Tuna program maalum kabisa ya kuwachukua vijana wetu kwa mujibu wa sheria lakini kwa kujitolea kwenda jeshini (JKT) na wanapokwenda kule wengi wanachukuliwa na taasisi zetu za ulinzi na usalama.”
Share:
Weka Maoni yako Hapa

Habari Zinginezo:

0 comments:

Post a Comment

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © 2025 GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger