Tuesday, May 3, 2016

Whatsapp yafungwa kwa saa 72 Brazil

Hakimu mmoja nchini Brazili amefunga mawasiliano ya mtandao wa simu kwa njia ya whatsapp kwa saa 72.Hakimu huyo Marcel Montalvao amesema kampuni inayomiliki mtandao huo imeshindwa kusaidia kutoa taarifa katika kesi ya uhalifu.

Mwezi Machi,Montalvao aliamuru kukamatwa kwa afisa mwandamizi wa Facebook katika nchi za Kilatini bwana Diego Dzoran baada ya kukataa kutoa ushirikiano katika uchunguzi dhidi ya dawa za kulevya.

Whatsapp mtandao unaomilikiwa na Facebook umesema umekatishwa tamaa na kitendo hicho kwa kuwa wamekuwa wakitoa ushirikiano wa kutosha mahakamani.

Mtandao huo umekuwa ukifungiwa mara kadhaa nchini Brazil kwa miezi michache ya karibuni kwa sababu zinazofanana na hizo.
Share:
Weka Maoni yako Hapa

Habari Zinginezo:

0 comments:

Post a Comment

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © 2025 GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger