Monday, April 25, 2016

Kifungo cha miaka 2....Ney kufanya juu chini kumtoa Siwema gerezani

 Staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ na mzazi mwenzake, Siwema Edson.
Staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ amefunguka kuwa yupo kwenye harakati za kumsaidia mzazi mwenzake, Siwema Edson (27) ambaye mwishoni mwa wiki iliyopita alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela kwa kosa la kujipatia mali kwa njia ya vitisho kutoka kwa kigogo mmoja serikalini aliyetajwa kwa jina moja la Deo.
 
Katika msala huo, Siwema alidaiwa kutoa vitisho kwa mlalamikaji akimtaka kumnunulia gari aina ya Honda CVR lenye namba za usajili T103 DDU lakini pamoja na kutimiziwa matakwa yake hayo, aliendelea kumtumia vitisho, akimtaka amtumie kiasi kikubwa cha fedha za mtaji, ndipo mlalamikaji akatoa taarifa polisi kisha mrembo huyo, akakamatwa ambapo mwishoni mwa wiki iliyopita alitupwa jela.

Akipiga stori na gazeti hili mara baada ya hukumu kutolewa mwishoni mwa wiki iliyopita Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Nay alisema tayari ameshatafuta mawakili wawili kwa ajili ya kukata rufaa ili kama itawezekana mama mtoto wake huyo arudi uraiani.
Share:
Weka Maoni yako Hapa

Habari Zinginezo:

0 comments:

Post a Comment

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © 2025 GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger