Saturday, April 30, 2016

Msanii Ally Nipishe Alazwa Ndani Miezi 3 Kwa Gari la Wizi

Msanii wa bongo fleva aliyekuwa akitamba na kibao cha 'My' Ally Nipishe aliswekwa ndani kwa miezi mitatu akikabiliwa na tuhuma ya kumiliki mali ya wizi kitu ambacho kilimpelekea kupotea katika game.

Akizungumza na Enewz Ally alikiri kukumbwa na shitaka hilo na kudai kuwa aliuziwa gari hiyo na mwanamke wake ambaye pia alikimbia baada ya sekeseke la polisi kuibuka.
  “Ni msichana ambaye nilikuwa na uhusiano naye na alikuwa akinisaidia kimaisha kitu ambacho sikutegemea kama angekuja kunifanyia tukio kama hili hata siku moja kwasababu nilikuwa namuamini sana ”, alisema Ally.
  Aidha Ally alisema kuwa tangu tukio hilo litokee wamemtafuta msichana huyo bila mafanikio ikambidi kutumia gharama nyingi zaidi kwaajili ya kulipa fidia kwa wenye mali ili kuimaliza kesi hiyo kuliko alivyowahi kusaidiwa na msichana huyo.
Share:
Weka Maoni yako Hapa

Habari Zinginezo:

0 comments:

Post a Comment

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © 2025 GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger