Friday, April 29, 2016

Colombia yahalalisha ndoa za jinsia moja

Mahakama ya Juu nchini Colombia imehalalisha rasmi ndoa za wapenzi wa jinsia moja nchini humo.
Hatua hiyo inaifanya Colombia kuwa nchi ya nne ya Amerika Kusini kuhalalisha ndoa hizo.

Wapenzi wa jinsia moja nchini Colombia awali tayari walikuwa wameruhusiwa kuungana na kuishi pamoja, na walipata manufaa mengi yanayohusiana na ndoa ikiwa ni pamoja na urithi, malipo ya uzeeni na marupurupu ya afya.
Lakini hawakuwa wameruhusiwa kufunga ndoa rasmi jambo ambalo sasa limefanyika.

Uamuzi huo ulitarajiwa kwa kiasi kikubwa baada ya uamuzi wa mahakama mapema mwaka huu wa kukataa pendekezo la kuwataka wathibitishaji wa mahakama kutosajili miungano ya wapenzi wa jinsia moja kama ndoa.
Share:
Weka Maoni yako Hapa

Habari Zinginezo:

0 comments:

Post a Comment

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © 2025 GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger