Tuesday, July 21, 2015

Taarifa ya kifo kwa vyombo vya habari


JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
Taarifa ya kifo kwa Vyombo vya Habari
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linasikitika kutangaza kifo cha Brigedia Jenerali Dismas Stanslaus Msilu (mstaafu) kilichotokea tarehe 19 Julai, 2015 katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo. 
Brigedia Jenerali Dismas Stanslaus Msilu (mstaafu) alizaliwa tarehe 24 September 1938 katika kijiji cha Mlolo, Kata ya Tanangozi, Wilaya ya Iringa Vijijini, Mkoani Iringa. Alijiunga na masomo ya Shule ya msingi na Sekondari na kuhitimu mwaka 1959. 
Marehemu Brigedia Jenerali Dismas Stanslaus Msilu alijiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania tarehe 01 Julai 1975. Alistaafu utumishi Jeshini tarehe 23 September 1993. 
Marehemu Brigedia Dismas Stanslaus Msilu ameacha mke na watoto. Mwili wa marehemu unatarajiwa kuagwa rasmi tarehe 22 Julai 2015 kuanzia saa 1:30 hadi 2:00 asubuhi katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo na mazishi yatafanyika Mkoani Iringa tarehe 23 Julai 2015.

MUNGU AILAZE MAHALI PEMA PEPONI ROHO YA MAREHEMU
BRIGEDIA JENERALI DISMAS STANSLAUS MSILU (MSTAAFU)
AMINA

Imetolewa na

Kurugenzi ya Habari na Mahusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P 9203, Dar es Salaam, Tanzania.
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 comments:

Post a Comment

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger