Samson Bwire mkazi wa Kitongoji cha Sango, Kata ya Nyasubi, Wilayani Kahama mkoani hapa ndiye baba mzazi anayedaiwa kutenda unyama huo uliopitiliza.
Uhai wa Devotha ulikatika Mei 16, mwaka huu saa nne usiku akiwa amezungukwa na jopo la madaktari waliokuwa wakiupigania uhai wake.

Baadhi ya madaktari waliokuwa wakimtibu walitokwa machozi wakati mtoto huyo akikata roho.
Mei 16, mwaka huu, majira ya jioni, Bwire ambaye ni polisi mstaafu alidaiwa kumcharanga mapanga mtoto wake huyo kisa kikidaiwa ni ugomvi uliotokana na wivu wa kimapenzi kati yake na mkewe, Happiness Elias (28).
Habari zinadai kuwa, katika ugomvi huo, mwanaume huyo alikuwa akimtuhumu mkewe kumsaliti. Hata hivyo, mkewe alifanikiwa kukimbia kusikojulikana.
Majirani walivunja mlango, wengine walipiga simu polisi ambao walifika na kumkamata mtuhumiwa.
Hata hivyo, Bwire hakuachwa salama kwani majirani hao wakiwa na hasira walimpiga sana.
Wakati mtuhumiwa akipelekwa polisi aliruka kutoka garini na kuangukia uso kitendo kilichomsababishia majeraha makubwa usoni.
Marehemu Devotha alizikwa Mei 17, mwaka huu mjini Shinyanga. Mama wa marehemu akizungumza kwa uchungu alisema: Maskini mwanangu amekufa kifo kibaya sana, wala hakuwa na hatia yoyote, naumia sana moyoni mwangu.
“Madaktari walipambana kuokoa uhai wake lakini Mungu akasema mwancheni aje kupumzika.”
0 comments:
Post a Comment