Tuesday, May 3, 2016

Watu Wawili Washikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya Kwa Kosa la Kupatikana na Bangi

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia mtu mmoja mkazi wa Matemela aliyefahamika kwa jina la HUSSEIN BAKARI (59) baada ya kukutwa na miche 25 ya Bangi akiwa amepanda kwenye bustani yake ya mbogamboga.
 
Mtuhumiwa alikamatwa katika msako uliofanyika mnamo tarehe 01.05.2016 majira ya saa 16:00 jioni katika Kijiji cha Mayota, Kata ya Lugelele, Tarafa ya Rujewa, Wilaya ya Mbarali, Mkoa wa Mbeya.
 
Aidha katika msako mwingine, Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la WILSON PHILIP (19) mwendesha Pikipiki/bodaboda, mkazi wa Msasani anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya akiwa na Bangi yenye uzito wa Gram 10.
 
Mtuhumiwa alikamatwa na askari katika msako uliofanyika mnamo tarehe 01.05.2016 majira ya saa 17:05 jioni huko Mtaa wa msasani, Kata ya Bagamoyo, Tarafa ya Tukuyu Mjini, Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya.
 
Watuhumiwa watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.
Imesainiwa na:
(EMANUEL G. LUKULA – ACP)
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 comments:

Post a Comment

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger