Friday, May 27, 2016

Video:Baada ya South Africa Kuplay Muziki wa Nyumbani kwa Asilimia 90, Diamond Kayaongea Haya

Baada ya South Africa kusema kuwa Media za Nyumbani zitaplay muziki wa nyumbani kwa asilimia 90, msanii toka Label ya WCB Diamond Platnumz amefunga mawazo yake.

Akizungumza na Ayo TV staa huyo alisema…‘Wasanii wanatakiwa kutengeneza nyimbo kali ili media mbalimbali ziweze  kuacha kucheza nyimbo za nje, kwa mfano zamani tulikuwa tukitoa baadhi ya video zinakubalika lakini sio kama video za nchi jirani lakini tulivyoanza kushoot video nzuri wenyewe wanaamini kuwa video za vijana wao ni kali’- Diamond Platnumz

‘Tukumbuke zamani watu walikuwa wanapenda sana movie za nchi za nje za kutoka East Africa, Nigeria na nchi zingine lakini walivyoanza wakina marehemu Kanumba, Ray kutengeneza movie soko lilikufa la watu wa nchi za nje tulikuwa tunapenda movie za kitanzania kwahiyo nasema tuache kulalamika tutengeneze kitu ambacho ni kizuri na kitapendwa zaidi kuliko kile cha nchi jirani’- Diamond Platnumz
Share:
Weka Maoni yako Hapa

Habari Zinginezo:

0 comments:

Post a Comment

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © 2025 GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger