Saturday, April 30, 2016

Sugu: 'Nyimbo itakayoizidi ‘Freedom’ itapata zawadi ya shilingi milioni tano'

Baada ya wimbo wa ‘Freedom’ kufanya vizuri kwenye media mbalimbali, Sugu anajipanga kuandaa shindano litakaloshindanisha nyimbo itakayoizidi wimbo huo.

Siku kadhaa zilizopita baada ya Sugu kuachia video ya wimbo wa ‘Freedom’ ulizua taharuki baada Mr Blue kulalamika kuwa Sugu kamuibia wimbo wake kabla ya uongozi wa studio ya MJ Record ambapo wimbo huo ulitayarishwa kuliweka sawa tatizo hilo.

Akizungumza kwenye kipindi cha FNL, kinachoruka kupitia EATV, Sugu amesema ‘tutaandaa shindalo la kushindanisha nyimbo itakayoizidi wimbo wa ‘Freedom’.

“Tumeshaongea na media moja ambayo tutapeleka wimbo wa ‘Freedom’ ambao wasanii wanaotaka watarekodi wimbo wataupeleka hapo. Kutakuwa na majaji kwenye shindano hilo watakao chagua nyimbo kumi bora na baadae kupata nyimbo moja. Mshindi kwenye shindano hilo atapata shilingi milioni tano,” aliongezea.
Sugu amesema kwenye shindano hilo halitabagua msanii yeyote kila mtu anaruhusiwa hata awe Mr Blue.
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 comments:

Post a Comment

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger