Friday, March 29, 2013

MWANAMITINDO FLAVIANA MATATA ATUMIKA KUTAPELI KWENYE MTANDAO WA FACEBOOK...!!

Mwanamitindo wa kimataifa, Flaviana Matata amekuwa akitumiwa na watu wasiojulikana kuwatepeli watu kupitia mtandao wa Facebook kwa akaunti yenye jina la Flaviana Matata’s huku ikidaiwa kuwa wengi wameshalizwa.

Taarifa ya Kampuni ya Compass Communications inayosimamia kazi za modo huyo inaeleza kuwa, watu hao wasiojulikana wamefungua akaunti kwenye mtandao wa Facebook na kuwarubuni watu kuwa, ‘Flaviana’ huyo anawatafutia kazi wasichana nje ya nchi kwa gharana ya shilingi hadi 200,000.
“Tunawatahadharisha watu kuwa Flaviana hatafutii wasichana kazi ya uanamitindo, wanaotumia akaunti ya Flaviana Matata’s ni genge la wahalifu, akauti sahihi ya Flaviana ni Flaviana Lavvy Matata,” ilieleza taarifa hiyo.
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 comments:

Post a Comment

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger