Thursday, March 28, 2013

Breaking Newzzzzz......NELSON MANDELA HOI HOSPITALINI

Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela amelazwa kwenye hospitali ambayo bado haijajulikana bado. Alilazwa jana usiku kutoka na maambukizi sugu ya mapafu.
mandela
Msemaji wa serikali Mac Maharaj amesema kwenye maelezo yake kuwa madaktari wanamhudumia vizuri na kwamba anapata matibabu yote yanayowezekana. Rais Jacob Zuma amemtumia salamu za ugua pole.
“Tunawaomba wananchi wa Afrika Kusini na duniani kote kumwombea mpendwa wetu Madiba na familia yake na kuwakumbuka kwenye fikira zao,” alisema Zuma kwenye maelezo yake.
Maharaj ameomba watu wawe na uelewa na kuwapa nafasi madaktari wafanye kazi yao. Mandela ana historia ya matatizo ya mapafu baada ya kuugua kifua kikuu mwishoni mwa miaka 27 aliyokuwa jela.
Share:
Weka Maoni yako Hapa

Habari Zinginezo:

0 comments:

Post a Comment

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © 2025 GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger