Wednesday, June 8, 2016

Video: Mabasi ya Mwendokasi Zaidi ya 30 Yamepata Ajali.....Zaidi ya Milioni 90 Zatumika Kuyatengeneza

Ajali za mabasi ya mwendokasi Dar es salaam zimeendelea kumake headlines ambapo leo June 8 2106 mbunge wa viti maalum CCM Amina Mollel amelifikisha bungeni na kutusaidia kuipata idadi ya mabasi yaliyopata ajali na kiasi cha fedha zilizotumika kufanya matengenezo.

Amina amesema…’Kwakuwa ajali nyingi zinasababishwa na madereva wazembe, mfano mzuri ukiwa ni Dar es salaam ambapo hadi sasa zaidi ya mabasi 30 yamepata ajali na gharama za matengenezo ikiwa ni zaidi ya milioni 90

Je, Serikali inatoa kauli gani kuwabana madereva wazembe wanaoisababishia hasara?

Majibu yametolewa na Waziri wa ofisi ya Rais tamisemi George Simbachawene ambapo amesema…’Babaraba zile ni kwa ajili ya mabasi yaendayo kasi na si vinginevyo, mtumiaji yoyote anayetumia barabara zile anakuwa amevunja sheria na hivyo yeye ndio anakuwa amegonga mabasi

Hawaruhusiwi kutumia barabara za mabasi yaendayo kasi zinazotumika sasa Dar es salaam, niwaombe waheshimu sana barabara hizo
Share:
Weka Maoni yako Hapa

Habari Zinginezo:

0 comments:

Post a Comment

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © 2025 GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger