SERIKALI inatarajia kuzindua mradi mkubwa wa kuboresha miundombinu ya
kusafirisha umeme Septemba mwaka huu, utakaomaliza tatizo la umeme
kukatika.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alisema kwa sasa
miundombinu ya kusafirishia umeme ni midogo na katika kuboresha hilo,
kuna mradi mkubwa utazinduliwa Septemba mwaka huu wa kusafirisha umeme.
Alisema mradi huo ni wa kusafirisha umeme kutoka kilovoti 220 hadi 400
kutoka Dar es Salaam-Tanga hadi Arusha na Iringa-Dodoma-Shinyanga, hivyo
tatizo la kukatika umeme litatatuliwa.
Waziri huyo alitoa maelezo hayo wakati akijibu swali la nyongeza la
Mbunge wa Korogwe Mjini, Mary Chatanda (CCM) aliyetaka kufahamu lini
umeme utakoma kukatika wilayani Korogwe.
Akielezea hilo, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani
alisema Serikali inafanya marekebisho ya transfoma na chanzo cha umeme
cha Hale mkoani Tanga ili kumaliza tatizo la kukatika umeme mara kwa
mara wilayani Korogwe na mkoani Tanga kiujumla.
0 comments:
Post a Comment