Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli amemteua mbunge wa jimbo la Ruangwa, Kassim Majaliwa kuwa waziri mkuu wa serikali ya awamu ya tano.
Uteuzi huo umetangazwa Bungeni alhamisi hii na spika wa bunge, Job Ndugai aliyesoma barua iliyoandikwa kwa mkono na Rais Magufuli.
Kabla ya hapo, mh Majaliwa alikuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri MkuuTawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( TAMISEMI).
Bunge limesimama kwa muda kupisha mchakato wa wabunge kuthibitisha uteuzi huo.
Mheshimiwa Majaliwa alizaliwa December 22, 1960.
0 comments:
Post a Comment