Thursday, January 24, 2013

BAADA YA IFM,T JOHNS NAO WAANDAMANA KUPINGA KUBAKWA NA KUIBIWA CHUONI


Wanafunzi wakiwa na mabango leo mjini dodoma.
ZAIDI ya wanafunzi 4000 wa Chuo Kikuu cha St. John’s kilichopo mjini DODOMA  wameandamana wakililalamikia Jeshi la Polisi Nchini kwa kushindwa kuthibiti vitendo vya matukio ya ubakaji na kulawitiwa yanayofanyika chuoni hapo.

Wanafunzi hao ambao waliandamana umbali wa kilomita tatu leo kutoka chuo kilipo na kuishia viwanja vya Mwalimu Nyerere walidai wanalenga kufikisha ujumbe kwa jamii kutambua vitendo vya kikatili vinavyofanyika chuoni hapo.
Maandamano hayo ambayo yalikuwa yakisindikizwa na
Polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia, yalipita katika mitaa mbalimbali ya Manispaa ya Dodoma.

Waandamanaji hao ambao mbali na kuimba nyimbo za kulilaumu Jeshi la Polisi kwa kushindwa kuthibiti vitendo hivyo, pia mabango waliyokuwa wamebeba yalikuwa yakililaumu jeshi hilo.
Askari jeshi la polisi wakijariobu kuwazuia wanafunzi leo mjini dodoma
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 comments:

Post a Comment

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger