Monday, March 20, 2017

Rais Magufuli Amkingia Kifua Makonda.....Amtaka Aendelee Kuchapa Kazi na Wala Asitishike na Kinachoendelea Mitandaoni



Rais John Magufuli amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuendelea kuchapa kazi na kwamba yeye hafanyii kazi maneno ya kwenye mitandao kwasababu yeye ndiyo Rais wa nchi hii.

Rais Magufuli amesema kuna baadhi ya watu wanaingilia majukumu yake wakati yeye ndiyo mwenye uamuzi na kwamba hapangiwi kazi ya kufanya kwa sababu anajiamini.

Mkuu huyo wa nchi amewataka wakazi wa Dar es Salaam kuchapa kazi ili kujiletea maendeleo badala ya kupoteza muda kufuatilia udaku kwenye mitandao.
"Watu wa Dar es Salaam tumejielekeza sana kwenye udaku ambao hausaidii maendeleo. Udaku ambao haumalizi hata foleni ya Dar.

"Ningefurahi sana huko kwenye mitandao kama tungekuwa tunajadili jinsi ya kufanya mambo ya maendeleo.
"Mimi sionyeshwi njia ya kupita na mtu. Njia ya kupita tayari nilishaonyeshwa na ilani ya chama changu.

"Kuandikwa kwenye mitandao hata mimi ninaandikwa, kwa hiyo nijiuzulu? Kuandikwa kwangu mimi siyo tija bali kuchapa kazi.
"Kuna wengine mmefikia hata hatua ya kunipangia. Nasema mimi ukinipangia ndio umeharibu
"Vitu ambavyo havina msingi vinachukua muda wetu mwingi sana. Mara upost hiki, mara uweke kile.

"Watanzania mjue kampeni zimeshakwisha. Ulie, ugaregare lakini Rais ni mimi John Pombe Magufuli na kwangu ni kazi tu.

"Mimi ni rais ninayejiamini, sipangiwi mambo ya kufanya. Hata fomu ya kugombea nilikwenda kuichukua peke yangu, kwa hiyo Makonda wewe chapa kazi," amesema Rais Magufuli.
Share:

Sunday, October 23, 2016

Aunty Fifi: Nimejipanga kwa Ubunge KIGOMA


MWIGIZAJI wa filamu Swahilihood Tumaini Bigilimana ‘Fifi’ amesema kwa sasa anajipanga kwa aajili ya kugombea Ubunge huko Kigoma ili aweze kuwasaidia wasanii wa filamu baada ya kilio chao cha muda mrefu kushindwa kutatuliwa kutoka na maharamia wa kazi zao hivyo anaamini kuwa endapo ataingia Bungeni kazi hyo itakuwa rahisi sana kutetea maslahi ya wasanii wa filamu Tanzania na wao wapate mtu wa kuwaongelea.

“Nijipanga kwa ajili ya kugombea ubunge mwaka 2020 jimbo nitalitaja baadae kwani nina lengo moja tu kuwa msemaji wa wenzangu yaani wasanii hususani wa filamu pamoja na wananchi wa jimbo langu lakini nihakikisha wasanii wa filamu tunafikisha ujumbe kwa ajili ya kupata maslahi zaidi,”alisema Fifi.

Fifi ambaye kwa sasa ni diwani kupitia chama cha ACT Wazalendo amesema kuwa wasanii wa muziki wamefanikiwa kwa kuwakilishwa na wasanii wenzao ambao ni waimbaji wakiingia bungeni inapotokea suala la maslahi yao wanasimamia kidete hivyo wana fursa nzuri kutetea muziki wao na kwenda mbali zaidi kwani wapo ndani.
Share:

Bodi ya Mikopo Ya Elimu Ya Juu Zanzibar Yasitisha Kutoa Mikopo Kwa Wanafunzi Vyuo Vikuu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein ameiagiza Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Zanzibar kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, kusimamisha utoaji wa mikopo ya elimu ya juu, hadi hapo serikali itakapojiridhisha na utaratibu mzima wa utoaji wa mikopo hiyo.

“Hatutatoa mikopo mwaka huu mpaka hapo tutakapokamilisha kazi ambayo tumeanza kuifanya ya kupitia upya utaratibu wa utoaji mikopo hiyo ili kuhakikisha inatolewa kulingana na mahitaji ya sasa ya nchi na kwa wanaostahili,” alisema Dk Shein.

Akizungumza katika hafla ya utoaji zawadi kwa wanafunzi waliofaulu daraja la kwanza katika mitihani ya Taifa ya Kidato cha Nne mwaka 2015 na Kidato cha Sita mwaka 2016, Dk Shein alisema kuwa katika utaratibu wa sasa wapo waliodanganya kupata mikopo na ambao wamekopeshwa lakini wamekuwa wagumu kurejesha mikopo hiyo.

Katika hafla hiyo, ambayo ilihudhuriwa pia na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Issa Haji Usii Gavu, jumla ya wanafunzi 119 waliomaliza kidato cha nne na wengine 50 waliomaliza kidato cha sita, walipewa zawadi kwa kupata daraja la kwanza katika mitihani yao ya taifa.

“Wako waliokejeli matokeo yenu, lakini ukweli ni huo mko 50 wa kidato cha tano mliopata daraja la kwanza na wengine 119 mliofaulu daraja la kwanza mtihani wa kidato cha nne,” alieleza Dk Shein na kuhoji msingi wa kukebehi matokeo hayo.

Aliongeza kuwa ufaulu wa wanafunzi hao, ni sifa kwa Zanzibar na anaamini kwa hatua zinazochukuliwa na serikali kuimarisha miundombinu ya elimu pamoja rasilimali watu kiwango cha ufaulu kitazidi kuongezeka.

“Mnapofanya mitihani sote tunakuwa na wasiwasi, nyinyi wenyewe, walimu, wazazi na sisi serikali kwa kuwa tunaelewa kuwa matokeo yoyote yale ni yetu sote kama ni mazuri ni furaha yetu sote na kama si mazuri ni huzuni yetu sote,” Dk Shein aliwaambia wanafunzi hao.

Dk Shein aliwataka wanafunzi hao kujivunia fursa waliyoipata na kuitumia vyema kujiimarisha kielimu, kwa kuwa haikuwa rahisi kabla ya Mapinduzi ya mwaka 1964 kuona vijana kutoka familia masikini wanapata fursa za kuingia sekondari kwa makundi.

“Mmepata bahati kubwa serikali yenu imeweka mazingira mazuri ya kupata elimu na haya ni matokeo ya utekelezaji wa ahadi ya Chama cha Afro-Shirazi na Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Sheikh Abeid Amaan Karume ya kutoa elimu bure itakaposhika madaraka,” Dk Shein alieleza.

Katika hatua nyingine, Dk Shein ametoa wito kwa walimu wakuu kuhakikisha kuwa wanasimamia vizuri walimu katika shule zao pamoja na kuwahimiza wakaguzi wa shule kutimiza wajibu wao ipasavyo.

Dk Shein alisema; “kumekuwepo na tatizo la usimamizi maskulini, hivyo serikali itatengeneza utaratibu wa kuwapatia motisha walimu wakuu na wakaguzi watakaofanya vizuri kwa kuwa ni dhahiri kuwa walimu wakuu wakisimamia vyema skuli zao na wakaguzi wakaifanya kazi yao ya ukaguzi kwa umakini tutapata matokeo mazuri zaidi.”

Katika salamu zake hizo kwa wanafunzi hao, ambao walisindikizwa na uongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, pamoja na walimu wakuu wa baadhi ya shule, Dk Shein aliwataka walimu kuongeza ari ya kufundisha na kwamba ni heshima na furaha ya mwalimu kuona mwanafunzi wake anapata matokeo mazuri.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimkabidhi zawadi Mwanafunzi Mahira Baraka Hamadi wa kidato cha sita Skuli ya Biashara Mombasa Wilaya ya Magharibi Unguja akiwa ni mwanafuzi aliyefanya vizuri katika Mtihani wa Taifa Mei mwaka 2016,hafla iliyofanyika jana Ikulu Mjini Unguja.
Share:

Majambazi Mengine Yauawa Katika Mapambano Makali Mkuranga




Jeshi la Polisi Mkoa wa Temeke limeua watu wanne wanaodhaniwa kuwa ni majambazi katika wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Temeke, Gilles Muroto alisema tukio hilo ni la Oktoba 21 baada ya polisi kupata taarifa za kuwepo kwa kundi la watu wanaodhaniwa ni majambazi.

Alisema baada ya taarifa, kikosi kazi cha Polisi cha Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, kilifanya ufuatiliaji na kubaini nyumba ambayo haijakamilika imezungushiwa uzio na muda wote mlango wa uzio huo ulikuwa umefungwa.

Aliongeza kuwa uchunguzi wa kina, ulifanyika na kubaini kuwa kweli kundi hilo, lipo ndani ya nyumba hiyo na kwamba muda mwingi mlango wa uzio, hufungwa na kuongeza kuwa majira ya saa tano askari wa kikosi kazi cha mkoa huo na mkoa wa Pwani, kilizingira nyumba hiyo.

“Baada ya kujipanga mlango wa uzio huo uligongwa na kutoa amri ya kuwataka walioko ndani ya nyumba hiyo wafungue mlango na kujisalimisha, lakini tulishangaa baada ya amri hiyo ghafla milio ya risasi ilianza kutoka ndani ya nyumba hiyo,” alisema Muroto.

Aliongeza kuwa baada ya milio hiyo, askari ambao walikuwa makini na wakiwa wamezingira nyumba hiyo wakiwa wamejipanga katika miundo ya mapigano, walianza mashambulizi kujibu mashambulio hayo.

Alisema majibizano yaliendelea na watu hao waliokuwa wanashambulia kutoka ndani, walivunja uzio na watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya watano walitoka huku wakiwa wanashambulia.

Muroto alisema askari waliendelea kupambana nao na kufanikiwa kuwajeruhi baadhi yao, na wengine walifanikiwa kutoroka na silaha zao.

“Mashambulizi kutoka ndani yalitulia na askari waliingia ndani ya uzio, kwa kuwa yalikuwa mapambano ya nguvu walikuta majambazi watatu wanaokadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 25 na 30 wakiwa wamejeruhiwa kwa risasi na hali zao zilikuwa mbaya na tuliwapeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili lakini walibainika kuwa tayari wameshakufa na miili yao imehifadhiwa hapo ikisubiri kutambuliwa,” alisema.

Alisema baada ya kufanya upekuzi, polisi walikuta silaha moja aina ya short gun pump action yenye MV.51516 R na namba ya usajili TZ car 99987 na risasi tano ndani ya magazini yake.

Risasi nyingine sita za short gun zilikutwa ndani ya mfuko wa plastiki pamoja na risasi nane za pistol.

Aidha alisema katika tukio hili, ilibainika kuwa kuna askari mmoja alijeruhiwa bega lake la kushoto na lilikuwa jeraha kubwa la risasi, hivyo alipelekwa katika Hospitali ya Muhimbili ambako amelazwa na anaendelea kupata matibabu akisubiri kufanyiwa upasuaji.

Muroto alisema ufuatiliaji wa majambazi, walitoroka eneo la mapambano uliendelea kwa kushirikiana na wananchi wa kijiji cha Mtambani, ambapo majira ya saa tatu asubuhi jambazi mmoja alipatikana akiwa mahututi na juhudi za kumfikisha hospitali zilifanyika. Hata hivyo, alikufa akiwa njiani.

”Tunawashukuru wananchi wote wema kwa ushirikiano mkubwa waliouonesha kwa Jeshi la Polisi, kwa kuliunga mkono katika kufichua wahalifu na kupambana na wahalifu, nitoe tahadhari kuwa mkoa huu ukifanya tukio ujue utashughulikiwa kabla hujakamilisha na ukifanikiwa kukamilisha azma yako haitachukua muda utakamatwa,” alisisitiza.
Share:

Madiwani CUF Watwangana Ngumi Hadharani ....Polisi Waingilia Kati


Polisi mjini Tanga jana walilazimika kuingilia na kuzima vurugu zilizotokea katika ofisi za Chama cha Wananchi (CUF), Wilaya ya Tanga zilizotokana na madiwani kugawanyika katika makundi mawili.

Makundi hayo ya madiwani yaligawanyika kuhusu uamuzi wa wenzao waliohudhuria kikao cha baraza la madiwani wa jiji hilo Oktoba 12.

Vurugu zilianza baada ya Mwenyekiti wa CUF wilayani humo, Rashid Jumbe ambaye pia ni diwani wa Mwanzage aliyegombea nafasi ya umeya kuamuru madiwani waliohudhuria baraza hilo watoke nje ili wajumbe waanze kumjadili mmoja mmoja.

Baada ya amri hiyo kundi la madiwani 12 waliotolewa nje kusubiri kuhojiwa waliamua kuingia kwa nguvu kutaka kumtoa Jumbe wakidai anasababisha makundi ndani ya chama hicho.

Vurugu ziliendelea kwenye mlango wa kuingilia, jambo lililosababisha wanachama waliokuwa nje kuingilia kati, huku wakirushiana ngumi.

Baadaye magari matatu ya polisi yaliwasili katika ofisi hizo na kuwatawanya wanachama waliokuwa wamejaa, jambo lililomsaidia Jumbe kufanikiwa kutoka.

Akizungumza baada ya vurugu hizo, Jumbe alisema kikao hicho kilikuwa na ajenda ya kuwahoji na kisha kuwajadili madiwani waliohudhuria baraza hilo kinyume na msimamo wa CUF.

Katibu wa CUF wa wilaya hiyo, Thobias Haule ambaye pia ni diwani wa Mnyanjani alisema madiwani waliohudhuria kikao cha baraza hawakwenda kinyume na chama kwa sababu waliamua kuwawakilisha wananchi waliowachagua, badala ya kuendeleza mgomo ambao hauwasaidii.

“Tukubali kwamba kwa kipindi cha mwaka mmoja tulichokaa bila kushiriki vikao vya baraza kuna mambo mengi ya maendeleo ya wananchi ambayo hayakufanyika, tumeamua kuhudhuria kwa masilahi mapana ya wananchi,” alisema Haule.

Mbunge wa Tanga Mjini, Mussa Mbarouk aliwataka wanachama wao kuwa wavumilivu kwa viongozi wako imara na hawatakubali kuyumbishwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba alisema Jumbe alifikishwa Kituo cha Polisi Chumbageni kuhojiwa kuhusu sakata hilo. Halmashauri ya Jiji la Tanga ina jumla ya madiwani 36; CUF inao 20 na CCM wako 16.
Share:

Saturday, October 22, 2016

MPENZI Mpya wa Wema Sepetu Afunguka, Adai Hamjui Idris Sultan


Model anayedaiwa kutoka kimapenzi na malkia wa filamu Wema Sepetu, Calisah amefunguka na kuzungumzia tetesi hizo ambazo zimekuwa zikisambaa katika mitandao ya kijamii.

Kijana huyo ambaye tayari ameshaonekana mara kadhaa katika baadhi ya video za mastaa wa muziki nchini, amemmwagia sifa malkia huyo wa filamu huku akishindwa kuweka wazi kama ni kweli anatoka naye kimapenzi au la!.

“Wema is a beautiful girl, sexy and every man’s dream, na mimi pia ni mvulana mzuri ambaye mwanamke yeyote angependa kuwa na mimi, akiwemo Wema mwenyewe,” Calisah alikiambia kipindi cha Enewz cha EATV. “Siwezi kusema moja kwa moja kwamba sisi ni wapenzi, lakini lakizima ujue kuwa Wema ni mzuri na mimi mzuri,”
Pia kijana huyo alidai kuwa hamtambui Idris Sultan na hakumbuki kama Tanzania imewahi kuwakilishwa na mtu anayeitwa Idriss katika mashindano ya Big Brother Afrika.

“Who? Idriss, kwani amewahi kuwa Big Brother? Which year?,”aliuliza kijana huyo. Malkia huyo wa filamu toka aachane na mshindi huyo wa Big Brother Afrika 2014, hajaweka wazi mahusiano yake mapy
Share:

Friday, October 21, 2016

Majambazi Hatari Wauawa.....Bunduki 9 Zakamatwa

Jeshi la polisi limedai kwamba limeua majambazi wawili hatari na kukamata bunduki tisa, kati ya hizo SMG saba, shotgun moja na riffle moja, risasi 473 na magazini 16 baada ya majibizano ya risasi katika misitu ya Milima ya Usambara, Kijiji cha Magamba wilayani Lushoto.

Katika majibizano hayo, pia polisi walidai kukamata bendera zenye maandishi ya lugha ya Kiarabu, redio saba za upepo na soksi za kuficha nyuso.

Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Polisi, Nsato Marijani alisema jana kuwa hiyo ilikuwa operesheni ya kuwasaka majambazi waliovamia Chuo Kikuu cha Sekomu, wilayani humo hivi karibuni.

Alisema katika tukio hilo, askari wawili walijeruhiwa kwa risasi. Marijani ambaye alikuwa katika milima hiyo inayodaiwa kuwa ngome ya majambazi hao, aliwataja waliouawa kuwa ni Mudrick Abdi (24) maarufu kwa jina la Osama, mkazi wa Mbagala Majimatitu Dar es Salaam na Sultan Abdallah (24) mkazi wa Kiembesamaki, Zanzibar.

Alisema askari waliojeruhiwa wanaendelea na matibabu na kwamba hawakupata madhara makubwa kwa kuwa walikuwa wamevaa majaketi ya kuzuia kupenya risasi .
Share:

Waziri Kairuki Afanya Ziara Dar, Kinondoni Kukagua Mradi Wa TASAF.......Asisitiza Waliotafuna Fedha Hizo Watatumbuliwa


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki amesema atahakikisha anawachukulia hatua watendaji wote, walioshiriki katika udanganyifu wa kuingiza kaya zisizostahili katika Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaosimamiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf).

Aidha, aliiagiza Tasaf kuhakikisha inafuatilia kaya zote ambazo ziliingizwa katika mpango huo bila kuwa na sifa zinazostahili, kwa kuziorodhesha kwa majina, wanapoishi na kiasi cha fedha walichopokea ili ripoti hiyo iwasilishwe kwa Rais John Magufuli.

Kairuki aliyasema hayo jana wakati akizungumza baada ya kupokea ripoti ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (Tasaf III) ya Mkoa wa Dar es Salaam, sambamba na kuzungumza na wananchi katika mitaa ya Kigogo Kati na Mikoroshoni, Manispaa ya Kinondoni.

“Kaya ambazo hazistahili hawafanyi peke yao wanashirikiana na watu, kama ni viongozi katika ngazi za mitaa na kata mitaa tunataka majina, na katika kila jina tujue nani alishiriki kumuingiza nani alikuwa akimchukulia na kama yupo mtumishi wetu wa umma tujue ni nani na hatua gani za kinidhamu zimechukuliwa.”

“...Msije mkashangaa nikaja kuelekeza polisi kukamata hawa na hawa kwa sababu hizi hela ni lazima zirudi,” alisema Kairuki.

Alisema ameshapokea taarifa za mikoa mbalimbali, lakini Dar es Salaam na wilaya zake bado na mwisho ilikuwa ni Oktoba 6, mwaka huu, lakini aliwaongeza wiki moja ambayo tayari imeisha na orodha hiyo inatakiwa ipelekwe kwa Rais Magufuli.

Kairuki aliongeza kuwa pamoja na mkoa kusema umeondoa kaya 789 ambazo hazina sifa, lakini kuna kaya 5,457 ambazo zinapaswa kuondolewa katika mpango huo kwa kuwa hazina sifa za kupokea ruzuku hiyo.

“...baada ya kuelekeza uhakiki wa nyumba kwa nyumba, sisi kwa taarifa tulizonazo tutaondoa kaya 5,457. Sasa ujiulize nyinyi ndio mlikuwa katika zoezi na mkapata idadi hiyo, hapa inaonesha kuna kitu hakipo sawa,” alisema.

Alisema katika kaya hizo zitakazoondolewa, 1,867 hazina vigezo vya umasikini, 563 zipo kwenye orodha lakini zilikuwa hazijitokezi kuchukua ruzuku na hazijulikani zilipo na kaya nyingine 2,114 hazikupatikana wala kujulikana zilipo wakati wa ukaguzi.

Alisema kaya hizi ni nyingi na hasa ikizingatiwa asilimia 76 hazijaingizwa katika mpango huo, hivyo kaya hizo ambazo ziliandikishwa zinapaswa kwenda kukaguliwa ili ziweze kuingizwa katika mpango huo ili katika awamu ya nane ya uhawilishaji fedha waweze kupata.

Kairuki alisema kiasi kikubwa cha fedha kimepotea, ambacho kingeweza kuwasaidia watu wanaostahili kuwa katika mpango huo.

Alisema wilaya za Kinondoni na Temeke zimeshapokea malipo ya awamu saba ambayo ni Sh bilioni 6.7. Alisema hadi sasa kuna kaya 32,456 zilizoondolewa kwenye mpango huo.

Kwa wastani kaya moja hulipwa kati ya Sh 20,000 hadi 60,000 kwa kutegemea idadi ya watu katika kaya.

Akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa alisema mpango huo ni muhimu kwa maendeleo ya taifa, lakini kuna watu wanaoharibu taswira ya Tasaf.

Alisema kuna fedha nyingi ambazo zinaishia kwenye mikono ya wajanja na haziwafikii walengwa wa mpango huo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Tasaf, Ladislaus Mwamanga alisema mpango huo umeandaliwa kitaalamu na utaendelea kuwa endelevu na kwamba mradi huo unategemea zaidi serikali na wafadhili, lakini hadi sasa kiasi kikubwa kimekuwa kikitoka kwa wafadhili.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala bora Mh. Angela Kairukia akiwa sambamba na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,akiendelea na ziara katika Mkoa wa Dar es salaam kukagua maendeleo ya mradi wa kusaidia kaya masikini TASAF
Share:

Watu 6 wanaswa na silaha kwa mganga wa kienyeji Mwanza


Taarifa Ya Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mwanza Kwa Vyombo


Kwamba Tarehe 18.10.2016 Majira Ya Saa 13:00hrs Katika Eneo La Buswelu Kata Ya Buswelu Wilaya Ya Ilemela Jiji Na Mkoa Wa Mwanza, Askari Wakiwa Katika Misako Na Doria Walifanikiwa Kuwakamata Watu Sita Wakiwa Na Silaha Mbili Zilizotengenezwa Kienyeji Pamoja Na Risasi Ishirini Na Tatu, Ambazo Walikuwa Wakizitumia Katika Matukio Ya Unyang’anyi Wa Mali Na Uporaji Hapa Jijini Mwanza Na Mikoa Mingine.

Aidha Tukio Hilo Limefanikiwa Baada Ya Kupokea Taarifa Kutoka Kwa Raia Wema Kuhusu Uwepo Wa Wahalifu Hao, Ndipo Askari Walifanikiwa Kumkamata Kwanza Jeremiah Maligia @ Mkumbo Miaka 25, Mnyiramba, Fundi Seremala Mkazi Wa Malega – Singida Ambaye Alipohojiwa Alikiri Kuhusika Na Kutaja Wenzake Waliokuwa Wakishirikiana, Na Kuwa Silaha Wamezificha Kwa Mganga Wa Kienyeji Aitwaye Leornad Litta @ Makai Anayeishi Mtaa Wa Kagida – Buswelu.

Askari Walikwenda Mahali Hapo Na Kufanikiwa Kumkamata Mganga Huyo Wa Kienyeji Bwana Leornad Litta Miaka 39, Akiwa Na Silaha Hizo Mbili Zilizotengenezwa Kienyeji Hapo Nyumbani Kwake Na Risasi Ishirini Na Mbili Zinazotumiwa Na Bunduki Ya Aina Ya Short Gun Na Risasi Moja Ya Rifle Aina Ya Mark Iv.

Aidha Katika Kuhojiwa Zaidi Na Askari Watuhumiwa Tajwa Hapo Juu Waliwataja Washirika Wao Wanne Ambao Walikuwa Wakishirikiana Katika Kufanya Uhalifu Ambapo Askari Walifanikiwa Kuwakamata, Ambao Ni 1. Kamgisha Jovini Kamhambwa Miaka 40, Mlinzi Na Mkazi Wa Iloganzala, 2. Juma Yusuph @ Jimi Miaka 35, Mkazi Wa Bwani Kinondoni, 3. Samweli Peter Miaka 36, Mkazi Wa Busweli Na 4. Shabani Hussein Miaka 26, Fundi Viatu Na Mkazi Wa Nyasaka Msumbiji.

Watuhumiwa Wote Walipofanyiwa Mahojiano Walikiri Kwamba Silaha Hizo Walizitumia Katika Unyang’anyi Wa Mali Na Uporaji Katika Maeneo Ya Jiji Na Mkoa Wa Mwanza, Aidha Jeshi La Polisi Kwa Sasa Linaendelea Na Uchunguzi Kuhusiana Na Tukio Hilo Na Matukio Waliyokuwa Wameyafanya, Pindi Uchunguzi Ukikamilika Watuhumiwa Wote Watafikishwa Mahakamani.

Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mwanza Naibu Kamishina Wa Polisi Ahmed Msangi Anatoa Wito Kwa Wakazi Wa Jiji Na Mkoa Wa Mwanza Akiwataka Kuendelea Na Tabia Ya Kutoa Ushirikiano Kwa Jeshi Lao La Polisi, Ili Tuweze Kudhibiti Uhalifu Katika Mkoa Wetu., Lakini Pia Anatoa Angalizo Kwa Wananchi Haswa Vijana Akiwataka Kuacha

Tabia Ya Kujihusisha Na Uhalifu Bali Wajikite Katika Kufanya Shughuli Halali Za Maendeleo, Kwani Jeshi La Polisi Lipo Vizuri

Kuhakikisha Ulinzi Na Usalama Upo Kwa Raia Wote Wa Jiji Na Mkoa Wa Mwanza.

Katika Tukio La Pili

Mnamo Tarehe 18.10.2016 Majira Ya Saa 14:00hrs Mchana Katika Eneo La Ilemela Wilaya Ya Ilemela Jiji Na Mkoa Wa Mwanza, Askari Walifanikiwa Kuwakamata Watu Wawili Ambao Ni 1. Rahim Feka Miaka 28, Mkazi Wa Ilala – Dar Es Salaam, 2. Ally Kawalale Miaka 32, Mkazi Wa Jetrumo – Arport Dar Es Salaam, Wakiwa Wanataka Kuuza Gari Lenye Namba T.778 Azv Aina Ya Toyota Land Cruiser Lililokuwa Wameliiba Huko Ilala Jijini Dar Es Salaam.

Aidha Watuhumiwa Hao Walikamatwa Baada Ya Kupokelewa Taarifa Ya Kuibiwa Kwa Gari Hilo Huko Dar Es Salaam Na Kwamba Kuna Uwezekano Kuwepo Eneo La Kanda Ya Ziwa, Ndipo Ulifanyika Upelelzi Kuhusiana Na Taarifa Hiyo, Na Kufanikiwa Kuwakamata Watuhumiwa Tajwa Hapo Juu Wakiwa Na Gari Hilo.

Watuhumiwa Wote Wapo Chini Ya Ulinzi Wa Jeshi La Polisi Wakiendelea Na Mahojiano , Huku Taratibu Za Kuwasafirisha Kwenda Dar Es Salaam Wakiwa Chini Ya Ulinzi Wa Askari Polisi Zikiwa Bado Zinaendelea.

Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mwanza Naibu Kamishina Wa Polisi Ahmed Msangi Anatoa Rai Kwa Wakazi Wa Jiji Na Mkoa Wa Mwanza Akiwataka Kuacha Tabia Ya Kununua Vitu Vya Wizi, Bali Pindi Wanapoona Biashara Za Wizi Zinataka Kufanyika Au Zinafanyika Watoe Taarifa Polisi Ili Watuhumiwa Waweze Kukamatwa Na Kufikishwa Mahakamani.

Katika Tukio La Tatu

Kwamba Tarehe 18.10.2016 Majira Ya Saa 23:00hrs Katika Kitongoji Cha Ibungiro Kijiji Cha Sagani Kata Ya Kandawe Wilaya Ya Magu Mkoa Wa Mwanza, Mtu Mmoja Msichana Aliyejulikana Kwa Jina La Dema Charles @ Bulayi Miaka 20, Mkazi Wa Kandawe, Ameuawa Kwa Kukatwa Na Vitu Vyenye Ncha Kali Sehemu Za Kichwani Na Kiunoni

Akiwa Amelalala Na Watu Wasiojulikana, Huku Wenzake Wa Wili Wakijeruhiwa Sehemu Mbalimbali Za Miili Yao.

Majeruhi Waliojeruhiwa Katika Tukio Hilo Ni 1.mariam Lucas @ Kapele Miaka 26, Mkazi Wa Kijiji Cha Sagani Aliyejeruhiwa Shingoni Na Kwenye Kiganja Cha Mkono Wa Kulia, 2. Kapelele Makubi @ Salulo Miaka 90, Ambaye Ni Baba Mwenye Nyumba/ Mji, Aliyejeruhiwa Mgongoni, Kichwani Na Kiunoni.

Inadaiwa Kuwa Wauaji Hao Walifika Katika Nyumba Hiyo Majira Tajwa Hapo Juu Na Kuwakuta Wenye Mji Wakiwa Wamelala, Ndipo Waliingia Ndani Na Kufanya Mauaji Hayo, Hadi Sasa Hakuna Mtu Yeyote Aliyekamatwa Kuhusiana Na Tukio Hilo.

Aidha Uchunguzi Wa Awali Umebainisha Kuwa Mauji Hayo Yametokana Na Kulipiza Kisasi, Jeshi La Polisi Kwa Sasa Lipo Katika Upelezi Pamoja Na Uchunguzi Kuhusiana Na Tukio Hilo, Majeruhi Wapo Katika Hospitali Ya Wilaya Ya Magu Wakiendelea Kupatiwa Matibabu Na Hali Zao Zinaendelea Vizuri.

Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mwanza Naibu Kamishina Wa Polisi Ahmed Msangi Anatoa Wito Kwa Wakazi Wa Jiji Na Mkoa Wa Mwanza Akiwataka Kutoa Ushirikiano Kwa Jeshi La Polisi Ili Watuhumiwa Wa Mauaji Hayo Wawezwe Kukamatwa Na Kufikishwa Katika Vyombo Vya Sheria
Share:

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Kufumuliwa.....Waziri Mwijage Asema Litaundwa Upya, Vijana 136 Kuajiriwa



WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amesema atalifumua na kuliunda upya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na kwamba wameshaanza kutafuta vijana 136 watakaoajiriwa katika shirika hilo kwa lengo la kudhibiti bidhaa, zinazoingizwa nchini chini ya viwango.

Aidha, wataweka kitengo maalumu kwa vijana hao, watakaokuwa na uwezo wa kuchunguza mipaka ya nchi, kunusanusa katika bandari bubu, kukamata, kuwasiliana na Polisi na kusimama mahakamani kutoa ushahidi.

Mwijage aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati wa utoaji wa tuzo kwa washiriki wa Programu ya Kaizen iliyo chini ya Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania.

Alisema lengo la kuiunda upya TBS ni kuhakikisha kwamba kazi zinafanyika ipasavyo ili kulinda viwanda vya ndani, vinavyozalisha bidhaa mbalimbali.

“Tutahakikisha kwamba hakuna bidhaa zitakazoingia bandarini bila ya kuwa na viwango vinavyotakiwa. Lengo ni kuwalinda walaji na viwanda vyetu, kwa nini tuagize vitu nje wakati viwanda vyetu vinazalisha bidhaa,’’ alisema Mwijage.

Hatua yake hiyo imekuja siku chache, baada ya makontena 100 kutoroshwa katika bandari kavu za Dar es Salaam bila ya kukaguliwa na hivyo kuikosesha mapato serikali na pia kuwa na hatari ya kuingiza bidhaa zilizo chini ya kiwango.

Akizungumza utekelezaji wa agizo la Mwijage na hadi Jumanne wiki hii kwa waliotorosha makontena hayo kujisalimisha, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dk Egid Mubofu alisema jana kuwa waziri ameongeza siku za utekelezaji wa agizo lake la kuwataka wafanyabiashara walioingiza maontena 100 bandarini bila kukaguliwa na TBS, watoe taarifa.

Dk Mubofu alisema baada ya agizo la awali, lililokuwa linamalizika Jumanne Oktoba 18, waziri aliongeza hadi leo ndipo hatua stahiki zichukuliwe.

Hata hivyo, alisema mwitikio umekuwa mkubwa na baada ya majumuisho ya leo, atakuwa katika nafasi nzuri ya kutoa taarifa kuhusu suala hilo.

Septemba 13, Mwijage alitoa siku nne kwa wafanyabiashara waliopitisha makontena 100 bandarini bila kukaguliwa na TBS, wakatoe taarifa katika shirika hilo.

Mwijage alisema wafanyabiashara ambao hawatajisalimisha baada ya kumalizika kwa siku hizo, hatua stahiki zitachukuliwa ikiwemo kulipa faini ya asilimia 15.

Akizungumzia Programu ya Kaizen, Waziri Mwijage alisema jambo linalotakiwa kwa sasa ni kuhakikisha kwamba viwanda vingi, vinakuwa na mfumo huo wa Kaizen, kwani utasaidia kuzalisha bidhaa bora na zenye viwango vya hali ya juu.

Alisisitiza lazima wafanyabiashara waboreshe bidhaa zao na kwamba wasitengeneze bidhaa kumtosheleza mteja bali kumridhisha mteja.

“Hatutaki kuingiziwa bidhaa ‘midabwada’ wala mataputapu, tunachotaka ni bidhaa zenye viwango vinavyotakiwa na tunataka wazalishaji wetu mzalishe bidhaa zenye viwango na viwango vya kimataifa kwa ajili ya kuuza nje ya nchi,’’ alifafanua.

Hata hivyo, alisema sababu ya viwanda kufa ni baada ya kufunguliwa milango ya bidhaa kutoka nje kuingia nchini, ambazo hazikukidhi viwango na kwamba wafanyabiashara kutoka nje walikuwa wanashindana na wafanyabiashara waliopo, ambao waliwekeza fedha nyingi katika miradi yao.

Kwa mujibu wa Mwijage, mpango huo wa Kaizen umefanywa katika mikoa mitatu ya Dar es Salaam, Morogoro na Dodoma ambapo umesaidia kuongeza tija katika uzalishaji na kupunguza upotevu wa malighafi.

Aidha, aliwataka Watanzania kupenda vitu vya nyumbani kwani wanahakikishiwa ubora na endapo vitakuwa na tatizo ni rahisi kuwabana wafanyabiashara wa ndani kuliko wa nje.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa JICA nchini, Toshio Nagase alisema mpango huo umesaidia kufundisha wakufunzi kwenye kampuni na viwanda zaidi ya 50 vilivyopo nchini.

Nagase alisema Kaizen imeleta matokeo kwa vitendo kwenye maeneo ya biashara kwa njia ya kusafisha eneo, kupunguza malighafi, kuhakikisha ubora wa bidhaa na kubadilisha tabia au motisha kwa wafanyakazi.

‘’Tunaamini kwamba Kaizen ni jambo muhimu katika kutengeneza viwanda vyenye ushindani kibiashara na kufanikisha lengo la kukuza viwanda kuelekea mwaka 2025,’’ alisema.

Alisisitiza kuwa mradi huo wa miaka mitatu, ulianza mwaka 2013 na kwamba ulianza Japan na nchi za Afrika unatekelezwa katika nchi za Ethiopia, Tunisia, Misri, Ghana, Zambia na Tanzania.

Share:

Kikosi Kazi Cha Jeshi La Wananchi (JWTZ) Cha Wasili Kagera Kwa Ajili Ya Kujenga Miundombinu Iliyoathiriwa Na Tetemeko La Ardhi


Kikosi kazi cha jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ)kutoka makao makuu ya Jeshi kimewasili Mkoani Kagera kwaajili ya ujenzi wa miundombinu ya serekali iliyoathiriwa vibaya na tetemeko la ardhi lililotokea Mkoana Kagera septemba 10 mwaka huu.

Akiongea wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa kituo cha afya katika kijiji cha Kabambyaile Kata ya Ishozi Wilaya ya Missenyi, Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salum Kijuu alisema kuwa kikosi hicho kinawataalamu wa fani zote za ujenzi na wamekuja na vifaa vyote vya ujenzi.

"Hiki kikosi kitafanya kazi kwa masaa 24 yaani watajenga usiku na mchana taasisi zote za umma zilizoathiriwa na tetemeko ikiwa ni pamoja na mashule na zahanati ili watoto waende shule na wagonjwa waendelee kupata matibabu"alisema.

Alisema mpaka kufikia july mwakani ujenzi wa miundombinu utakuwa umekamilika kwa robo tatu na aliwataka wananchi wawape ushirikiano maeneo yote watakayopita kujenga miundombinu ya umma.

Kiongozi wa kikosi hicho Meja Buchadi Kakura alisema kuwa kikosi hicho kimekuja Kagera kusaidia serekali ya Mkoa kurudisha miundombinu yote ya umma iliyoathiriwa na tetemeko la ardhi katika hali yake ya kawaida.

"Ni vigumu kusema lini tutakamilisha ujenzi ila sisi tutafanya kazi usiku na mchana ili ujenzi huu ukamilike ndani ya muda mfupi"Alisema Meja Kakura.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salimu Kijuu(mwenye Suti)akisikiliza maelezo juu ya kikosi kazi cha askari waliokuja kujenga miundo mbinu ya umma iliyoathiriwa na tetemeko la ardhi
Share:

Wadau wa haki za binadamu nchini waendelea kusisitiza adhabu ya kifo ifutwe

Licha ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutotekeleza adhabu ya kifo kwa zaidi ya miaka 20. Imeendelea kusisitizwa kuifuta sheria ya adhabu ya kifo kwa watuhumiwa wa makosa ya mauaji kwa kuwa haisaidii kupunguza makosa hayo na kwamba iangalie chanzo cha tatizo hilo kwa lengo la kufanyia marekebisho.

Ushauri huo umetolewa jana na wadau mbalimbali wa haki za binadamu katika kongamano la kuijadili adhabu ya kifo nchini, lililoandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa (UN).

Wadau hao walisema kuwa, falsafa ya ukuaji wa adhabu huzingatia vigezo viwili ambavyo ni kutoa funzo kwa jamii pamoja ma kumrekebisha mkosaji. Wadau hao waliitumia hoja hiyo kuisisitiza serikali kufuta adhabu ya kifo kwa kuwa endapo mtuhumiwa akiuawa hatopata fundisho na pia kifo chake kinatafsiriwa sawa na kosa hilo kujirudia.

Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Hellen Kijo-Bisimba alisema kituo hicho hakitaacha kuishauri serikali kuifuta adhabu hiyo kwa kuwa haisaidii kutokomeza matukio ya mauaji na pia huenda ikaathiri watu wasio na hatia.

“Inabidi serikali iangalie chimbuko la matukio ya mauaji ili litokomezwe na si kuhukumu watu kwa adhabu ya kifo, hatumaanishi wasihukumiwe bali watafutiwe adhabu nyingine kwa kuwa tangu kuanza kutumika adhabu hii matendo ya mauaji hayajapungua,” alisema.

Aliongeza kuwa ” Kumuua mtu si suluhisho bali kosa hilo linazidi kufanyika na si sahihi. LHRC tunaendelea kuipinga adhabu hii sababu haisaidii kupunguza mauaji,”

Bisimba alidai kuwa, asilimia kubwa ya wanaohukumiwa adhabu ya kifo ni watu wasio na kipato na kwamba hali hii huonyesha adhabu hiyo hutekelezwa kitabaka zaidi.

Mwakilishi wa UN, Roeland Van de Geev alisema kuwa shirika hilo halitailazimisha serikali kuifuta sheria hiyo bali litawezesha mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO’s) yanayohusika na haki za binadamu nchini kuishauri serikali kufuta adhabu hiyo.

“Nchi zaidi ya 140 duniani zimefuta adhabu hiyo, na hakuna matukio ya kutisha ya mauaji katika nchi husika, mfano Marekani inatekeleza adhabu ya kifo lakini matukio ya mauaji bado yanaendelea. Hii inamaanisha kwamba suluhu pekee ni kutibu au kuzuia vyanzo vya matukio hayo,” alisema.

Alishauri kuwa “Adhabu hii hafai kutekelezwa sababu inaondoa utu wa mtu. Tanzania pamoja na nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki zifute sheria hiyo.”

Bahame Tom Nyanduga kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora alisema adhabu hiyo haistahili kuendelea kutekelezwa nchini kutokana kwamba ilianzishwa na wakoloni kwa lengo la kulinda utawala wao.

“Haki ya binadamu ya kuishi ndiyo msingi wa haki nyingine, katiba ya 1977 inatambua haki ya kuishi. Mahakama haiwezi futa adhabu hii bali serikali ndiyo yenye wajibu wa kuifuta sheria hiyo hivyo ni vyema ikafanya hivyo,” alisema.

Alisema ingawa serikali haijatekeleza adhabu hiyo kwa zaidi ya miaka 20 lakini inawajibu wa kuifuta sababu watu wanazidi kuhukumiwa.

“Nchi zaidi ya 20 Afrika zimefuta adhabu hii na hatusikii kama kuna kukithiri kwa matukio ya mauaji.Ni vigumu kuhusisha adhabu ya kifo kama suluhisho pekee la kutokomeza mauaji,” alisema.

Sheikh Ally Hemko kutoka Baraza Kuu la Waisilamu Tanzania (Bakwata) alishauri jamii kuepukana na vitendo vya mauaji kwa kuwa dini hairuhusu.

“Dini yetu hufundisha kuwa mtu anayeua nae aue ingawa pia inasisitiza kuua ni dhambi hivyo ili kuondokana na utata huo, jamii inawajibu wa kuacha vitendo hivyo sababu hata kama sheria hiyo ikifutwa watu wasio wema watazidi kuua,” alisema.
Share:

TSNP kutinga kwa Dk. Ndalichako, wapanga kutoa tamko la kupinga vigezo vya kupewa mkopo



Mtandao wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania ( TSNP) umepanga kuunda kamati ya viongozi wa serikali za vyuo vikuu ili kukutana kwa dharura na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk. Joyce Ndalichako.

Pia imepanga kuandaa tamko la kupinga tamko la mabadiliko ya vigezo vitakavyozingatiwa katika utoaji mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu, lililotolewa hivi karibuni na Naibu Waziri wa Elimu Mhandisi Stella Manyanya.
Mtandao huo umedai kuwa, mabadiliko hayo ya vigezo yamesababisha wanafunzi wengi kukosa mikopo huku baadhi yao kupunguziwa fedha za kujikimu.

Mkurugenzi wa Haki za Wanafunzi TSNP, Venancy Shitindi jana alisema kuwa TSNP kwa sasa inakusanya taarifa za changamoto zinazo wakabili wanafunzi waliokosa mikopo ili kuandaa tamko la kupinga mabadiliko hayo, litakalo pelekwa katika Ofisi ya Rais, Waziri Mkuu na Wizara ya Elimu.
“Tumepanga kutengeneza kamati ndogo ya viongozi kwa ajili ya kukutana kwa dharura na waziri mwenye dhamana ya elimu ili kutoa malalamiko ya wanafunzi juu ya vigezo vipya vilivyotolewa na wizara yake, pia tunakusanya taarifa na kuandaa tamko tutakalolisambaza katika ofisi ya rais, wizara ya elimu na ofisi ya waziri mkuu,” alisema.

Alidai kuwa, mtandao huo umefanya utafiti wa vigezo vipya vilivyotajwa na kubaini kuwa haviendani na sera ya elimu ya mwaka 2014, wala ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) pamoja na mpango mkakati wa kitaifa wa maendeleo kama alivyosema Mhandisi Manyanya katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari.

“Baada ya kusoma taarifa ya Naibu Waziri Manyanya tulikwenda kuangalia sera ya elimu ya mwaka 2014, tukakuta hakuna sehemu iliyoainisha kundi linalostahili kupata mkopo bali imeeleza elimu itolewe bure na mikopo itolewe kwa kila mwanafunzi. Na kwamba elimu imepewa kipaumbele cha kuleta maendeleo katika nyanja zote haijasema kwa wanaosomea masomo ya sayansi pekee,” alisema na kuongeza.

“Hata mpango wa maendeleo wa miaka 5 yaani 2025, unaeleza kuwa Tanzania inatakiwa kuwa na uchumi wa kati na kwamba imetoa kipaumbele elimu kutolewa bure kwa nyanja zote ili wapatikane wataalamu wa fani mbalimbali na wa kutosha.”

Hata hivyo, taarifa iliyotolewa na Mhandisi Manyanya ilisema kuwa serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, huandaa sifa na vigezo vya utoaji Mikopo kila mwaka ili kuendana na malengo na matarajio yaliyopo katika mipango na mikakati ya kitaifa kama ilivyoainishwa katika Dira ya Taifa 2025.

Na kwamba Serikali imetoa vipaumbele katika utoaji mikopo kwa wanafunzi wa mafunzo ya Fani za Sayansi za Tiba na Afya,Ualimu wa Sayansi na Hisabati, Uhandisi wa Viwanda, Kilimo, Mifugo, Mafuta na Gesi Asilia, Sayansi Asilia na Mabadiliko ya Tabianchi, Sayansi za Ardhi, Usanifu Majengo na Miundombinu.
Share:

Thursday, October 20, 2016

Polisi Feki Akamatwa Jijini Mwanza


VIDEO HAPO CHINI

Share:

Singeli Imenipa Nyumba na Gari – Man Fongo


Msanii wa muziki wa Singeli nchini Man Fongo amefunguka na kusema anashangaa mafanikio makubwa ambayo ameyapata ndani ya muda mfupi kupitia muziki wa Singeli hususani kupitia kazi yake ya ‘Hainaga ushemeji’ ambayo imemtambulisha vyema kwa jamii.

Man Fongo kupitia kipindi cha Planet Bongo ya EATV alisema kuwa muziki huo umebadilisha maisha yake ndani ya muda mfupi na sasa anaona maisha kwake ni kama mepesi akilinganisha na kipindi cha nyuma.

“Kupitia Singeli saizi nimepanga nyumba nzima Tabata, nina miliki gari yangu Toyota Altezza , unajua haya kwangu ni mafanikio yaliyokuja kwa muda mfupi sana kutoka kuishi gheto chumba kimoja mpaka sasa naishi nyumba nzima, familia saizi inaniangalia mimi hivyo naweza kusema Singeli ina neema sana kwangu na mafanikio kwangu yamekuja haraka mpaka nashangaa” alisema Man Fongo
Share:

Become a Fan

Popular Posts

Copyright © GUMZO LA JIJI | Powered by Blogger